Alphonce Mabula atambulishwa JS kabyile
Kiungo wa Kimataifa wa Tanzania, Alphonce Mabula Msanga ametambulishwa rasmi kama mchezaji mpya wa klabu ya JS Kabylie ya Nchini Algeria kwa uhamisho huru baada ya mkataba wake na klabu ya Şamaxı FK ya Azerbaijan kusikia ukomo.
Klabu hiyo imethibitisha kukamilisha usajili wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 leo Agosti 31, 2026 kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii bila kuweka wazi urefu wa mkataba wake klabuni hapo.
