Maua Sama kuwa mama mtarajiwa
Msanii wa Bongo Flava Maua Sama ameamua kuwafahamisha mashabiki zake kuwa anatarajiwa kuwa mama hivi karibuni baada ya ku-share picha zake mpya ambazo zimemuonyesha akiwa mjamzito baada ya tetesi kusambaa mitandaoni.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Maua ameweka picha hizo akisindikiza na ujumbe uliosomeka, “Am grateful Alhamdulillah, post ambazo imepata comments mbalimbali za wasanii na mashabiki zake wakimpa hongera na kumtakia kheri.
