Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2026

Maxi Nzengeli avunja rekodi ya Kelvin Nashon

Picha
Max Nzengeli ametumia mechi 5 tu kutwaa tuzo 4 za Mchezaji Bora wa Mechi, akivunja rekodi ya Kelvin Nashon aliyetwaa akiwa Pamba Jiji. Msimu uliopita, Nashon alikuwa miongoni mwa wachezaji wanne (4) waliochukua tuzo nyingi msimu uliopita. Max anahitaji tuzo moja tu kuvunja rekodi ya Feisal na Okello, waliokusanya tuzo 5, wakiwa miongoni mwa wachezaji waliochukua tuzo nyingi zaidi, nyuma ya kinara Clatous Chama aliyechukua tuzo 7. Okello na Feisal walitumia zaidi ya michezo 15 kutwaa tuzo 5 msimu mzima, wakati Max ametumia mechi 5 tu.

Libasse Gueye aingia anga za Bruno Fernandez na Pedro Gonzalez

Picha
Manchester wana Bruno Fernandes Barcelona wana Pedri Gonzalez Man City wana Rayyan Cherki Madrid wana Arda Guller Simba wana Libasse Gueye, laiti kama Simba ingelikuwa Taifa basi Gueye angelikuwa " National treasure halisi ya kutumainiwa inayopaswa kutunzwa kwa hali na Mali. Gueye mpaka sasa amecheza mechi tano na amefanikiwa kutia assist tano ikiwa ni mwendelezo mzuri kwake msimu huu

Azam FC na Simba sasa kupigwa Septemba 16

Picha
Mechi ya Simba dhidi ya Azam iliyopangwa kuchezwa baada ya Simba kumalizana na Mighty wanderers mkondo wa kwanza ligi ya mabingwa umeahirishwa na sasa utapigwa tarehe 16 baada ya Simba kumalizana na Mighty mkondo wa pili Mliosubiria kumuona maestro Feitoto akicheza dhidi ya Simba mtasubiri kidogo

Jayrutty yabisha hodi Rayon Sports

Picha
Kampuni ya Kitanzania Jayrutty Investment East Africa Ltd inaendelea kupanua ushawishi wake katika sekta ya michezo barani Afrika kupitia ushirikiano na klabu mbalimbali. Kwa upande wa Rayon Sports ya Rwanda, Jayrutty imeingia makubaliano ya miaka mitano ya kuwa mshirika rasmi katika usambazaji wa jezi na vifaa vya klabu hiyo, katika mkataba unaoripotiwa kuwa na thamani ya Dola milioni 3.5. Rayon Sports pia imeonekana ikitumia jezi mpya za Jayrutty wakati wa safari ya kuelekea Cameroon, huku kampuni hiyo ikishirikiana na Umbro katika utengenezaji wa jezi hizo. Jayrutty pia ina uhusiano wa kibiashara na Simba SC, ikiwa miongoni mwa kampuni zinazojihusisha na mavazi pamoja na bidhaa za michezo. Hatua hizi zinaendelea kuifanya Jayrutty kuwa miongoni mwa kampuni za Kitanzania zinazojenga ushawishi katika sekta ya michezo nje ya mipaka ya Tanzania. Kutoka Tanzania hadi Rwanda na katika soka la kimataifa Jayrutty inaendelea kujenga jina barani Afrika.

Yanga, Simba na Gor Mahia uwanjani mwishoni mwa wiki Ligi ya mabingwa Afrika

Picha
Msimu wa CAF Champions League unaanza kwa vigogo wa Tanzania; Yanga SC na Simba SC wakiwa tayari kwa hatua ya kwanza ya mchujo. Yanga itakuwa ugenini kukutana na Gaborone United, huku Simba wakikabiliana na Mighty Wanderers nao wakiwa ugenini. Majirani Gor Mahia wao watawakaribisha Pyramids FC kutoka Misri na mechi GABORONE UNITED YANGA SC Jumamosi, 5 Septemba Saa 1:00 Usiku Azam Sports 2 HD MIGHTY WANDERERS SIMBA SC Jumapili, 6 Septemba Saa 9:00 Alasiri Azam Sports 2 HD

Messi atandika daruga

Picha
Shirikisho la Soka la Afrika Kusini (SAFA) limemtambulisha rasmi mkufunzi Pitso Mosimane kuwa kocha mkuu mpya wa Timu ya Taifa ya Afrika Kusini, (Bafana Bafana) akichukua mikoba ya Hugo Broos aliyeondoka baada ya mkataba wake kutamatika. Rais wa SAFA, Danny Jordaan, amemtangaza rasmi Mosimane leo Septemba 1, 2026 ikiwa ni urejeo wa pili kwa kocha huyo wa zamani wa Mamelodi Sundowns na Al Ahly kuinoa Bafana Bafana tangu alipokiongoza kikosi hicho kuanzia 2010 hadi 2012.

Pitso Mosimane awa kocha mkuu Bafana Bafana

Picha
Shirikisho la Soka la Afrika Kusini (SAFA) limemtambulisha rasmi mkufunzi Pitso Mosimane kuwa kocha mkuu mpya wa Timu ya Taifa ya Afrika Kusini, (Bafana Bafana) akichukua mikoba ya Hugo Broos aliyeondoka baada ya mkataba wake kutamatika. Rais wa SAFA, Danny Jordaan, amemtangaza rasmi Mosimane leo Septemba 1, 2026 ikiwa ni urejeo wa pili kwa kocha huyo wa zamani wa Mamelodi Sundowns na Al Ahly kuinoa Bafana Bafana tangu alipokiongoza kikosi hicho kuanzia 2010 hadi 2012.

Waamuzi wanne wa Tanzania kuchezesha Ligi ya mabingwa Afrika

Picha
Waamuzi wa Tanzania Nasir Salum, Mohamed Mkono, Ally Ramadhani na Ahmed Arajiga wameteuliwa na CAF kuchezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) JS Saoura (Algeria) vs Horoya AC ( Guinea) utakaochezwa uwanja wa Miloud Hadefi Septemba 4, 2026

Ibrahim Doumbia ashukuru mashabiki Simba

Picha
Mchezaji wa Simba SC, Ibrahim Doumbia, amesema ameguswa sana na upendo na sapoti aliyopewa na mashabiki wa timu hiyo baada ya kushuka kwenye basi na kukutana na bango lenye ujumbe “WE ARE TOGETHER DOUMBIA. WE LOVE YOU.” Doumbia amesema tukio hilo lilimgusa kiasi cha kumfanya kutokwa na machozi, akieleza kuwa katika soka kuna nyakati ngumu, ushindi, vipigo, lawama na wakati mwingine mashaka, lakini mashabiki wa Simba wamemkumbusha jambo moja muhimu kuwa hayuko peke yake. Amesema mashabiki wote wa Simba tayari wana nafasi kubwa moyoni mwake na amewahakikishia kuwa ataendelea kufanya kazi kwa bidii, kupambana na kutoa kila alicho nacho kwa ajili ya jezi ya Simba. “Nyakati hizi ngumu, In Shaa Allah, tutazishinda pamoja. Familia haitelekezi kila mmoja wakati wa changamoto. Familia hubaki pamoja, huinuka na kusonga mbele pamoja.” Doumbia pia amewashukuru mashabiki wa Simba kutoka Tanzania nzima, wakiwemo wanaomhimiza, wanaomuombea, wanaomuamini pamoja na wanaomkosoa, akisema anawapenda wote ...