Maxi Nzengeli avunja rekodi ya Kelvin Nashon
Max Nzengeli ametumia mechi 5 tu kutwaa tuzo 4 za Mchezaji Bora wa Mechi, akivunja rekodi ya Kelvin Nashon aliyetwaa akiwa Pamba Jiji. Msimu uliopita, Nashon alikuwa miongoni mwa wachezaji wanne (4) waliochukua tuzo nyingi msimu uliopita. Max anahitaji tuzo moja tu kuvunja rekodi ya Feisal na Okello, waliokusanya tuzo 5, wakiwa miongoni mwa wachezaji waliochukua tuzo nyingi zaidi, nyuma ya kinara Clatous Chama aliyechukua tuzo 7. Okello na Feisal walitumia zaidi ya michezo 15 kutwaa tuzo 5 msimu mzima, wakati Max ametumia mechi 5 tu.