Yanga mwendo mdundo ikiilalua Pamba Jiji

Timu ya Yanga SC usiku huu imeendelea kuchanja mbuga kufuatia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Pamba Jiji ya Mwanza katika mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa KMC Complex Mwenge jijini Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo Yanga inaendeles kukaa kileleni ikifikisha pointi 12 huku ikiwa imefunga mabao 13 huku ikicheza mechi 4.

Yanga ilianza kupata bao kupitia kwa Maxi Nzengeli assist ya Sheikh Ibrahim Toure dakika ya 17 kabla ya Toure kufunga la pili assist ya Peter Shalulile dakika ya 23.

Yanga sasa itasafiri tarehe 1, Septemba kuwafuata Fountain Gate wanaotumia uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha.




Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI