Oruma aiponda Yanga, aifagilia Simba
Mchambuzi wa michezo Wilson Oruma ametoa kauli nzito kuhusu ubora wa kikosi cha Yanga SC, akidai kuwa timu hiyo haina kikosi cha kutosha kwa ushindani wa msimu huu.
Oruma ameenda mbali zaidi kwa kutoa utabiri kwamba Simba SC itatwaa ubingwa, akiamini itakuwa na tofauti ya pointi 10 mbele ya Yanga.
Kauli hiyo imeibua mjadala miongoni mwa mashabiki wa soka, huku msimu ukiwa bado katika hatua za mwanzo na timu zikiendelea kupambania alama.
