Kocha Geita Gold aizimia Simba
Kocha wa Geita Gold, Zubery Katwila, amesema kesho wanakutana na timu bora ambayo inaendelea kuimarika zaidi kiuchezaji dimbani.
Katwila amesema kadri siku zinavyosonga, Simba inaendelea kuwa bora zaidi, hivyo wao kama Geita Gold wamejiandaa na mbinu zitakazowasaidia kufanya vizuri.
Pia amesema watajaribu kutumia makosa ambayo Simba itafanya ili kuwapa adhabu uwanjani na kutafuta matokeo mazuri.
