Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TAMBWE, KAZE SASA KUKIPIGA SIMBA, MOTO WAO UTAWAKA DHIDI YA OLJORO

Hatimaye wachezaji wapya wa Simba kutoka Burundi mshambuliaji Amisi Tambwe na beki Gilbert Kaze (Pihani) kutoka Burundi, jana walipata uhamisho wa kimataifa kwa ajili ya kuanza kuichezea klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, ilielezwa jijini Dar es Salaam jana.


Tambwe na Kaze juzi Jumamosi walishindwa kuitumikia timu yao hiyo kutokana na kukosa ITC na kusababisha mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, juzi asafiri kwenda Burundi kukamilisha usajili wa wachezaji hao.

Tambwe na Kaze waliwasili nchini wiki iliyopita na siku iliyofuata walielekea Kahama, Shinyanga kuungana na wachezaji wengine wa Simba ambao walikuwa wameweka kambi mkoani humo kujiandaa na msimu mpya wa ligi ulioanza Jumamosi.

Akizungumza na mtandao huu, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema kuwa tayari wamekamilisha uhamisho wa wachezaji hao na keshokutwa Jumatano watashuka uwanjani kuitumikia timu hiyo kwa mara ya kwanza watakapoivaa JKT Oljoro kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

"Tumekamilisha mchana huu (jana mchana), Jumatano watacheza, tunashukuru tumewapata," alisema Mtawala.

Alieleza kwamba usajili huo umefanikishwa na safari ya mwenyekiti, Ismail Aden Rage, ambaye juzi alilazimika kusafiri hadi Burundi kwenda kukamilisha usajili huo kufuatia 'siasa' kuanza kuingia baada ya nchi hiyo kuona kwamba itawakosa wachezaji hao katika mechi za mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) zitakazofanyika mapema mwakani.

Aliongeza kuwa suala la Betram Mwombeki na klabu yake ya zamani ya Pamba ya jijini Mwanza pia limefanyiwa kazi kwa kuwapa Sh. milioni mbili ili kubariki uhamisho huo.

Aliwataka mashabiki wa Simba kuwa na utulivu na matokeo mazuri yatapatikana katika timu yao.
Simba ilianza kwa sare ya magoli 2-2 dhidi ya Rhino Rangers ambayo imepanda daraja na kucheza Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu ilipoanzishwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa