Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NWOFOR WA NIGERIA AJIUNGA NA SC HEERENVEEN

Timu ya taifa ya Nigeria
Mshambulizi wa kimataifa wa Nigeria Uche Nwofor amejiunga na klabu ya Uholanzi ya SC Heerenveen, kwa mkpo kutoka kwa klabu ya VVV Venlo iliyoshushwa daraja.

Nwofor mwenye umri wa miaka 21, ambaye alikataa ombi kutoka kwa vilabu vya Urussi na Uturuki, alisaini mkataba wake mpya baada ya kukamilisha uchunguzi wa kimatibabu mapema hii leo.
Aliifungia timu ya taifa ya Nigeria Super Eagles magoli mawili wakati ilipoilaza Afrika Kusini ka magoli mawili kwa bila wiki mbili zilizopita mjini Durban.
Akiongea na BBC Nwofor alisema, amefurai kusaini mkataba mpya kwa kuwa atapata fursa ya kuimarisha kipaji chake.
''Nitaendelea na masomo yangu ya taalumu ya mchezo wa soka nchini Uholanzi na naamini nimepata klabu inayonifaa'' Alisema mchezaji huyo.
Nwofor ambaye ameweka rekodi ya kuwa mmoja wachezaji wanaofunga magoli, katika kikosi cha wachezaji chipukizi nchini Nigeria, alijiunga na Venlo Septemba mwaka wa 2011 na kufunga magoli kumi na tatu baada ya kucheza mechi hamsini na mbili.
Vilabu bya Arsenal, Tottenham na Newcastle vimehusishwa na mchezaji huyo ambaye amefananishwa na mshambulizi matata wa Aston Villa Christian Benteke.
Mchezaji huyo alikataa kujiunga na klabu ya CSKA Moscow Januari mwaka huu, kwa kitita cha pauni milioni nne na meneja wake Tonny Harris amesema anaimani kuwa mchezaji huyo amechukua uamuzi unaofaa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa