Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHEKA NA MMAREKANI WAKE KUPIMA UZITO LEO



Mabondia Francis Cheka (Pichani) kutoka Morogoro na Phil William wa Marekani wanatarajia kupima uzito leo kujiandaa na pambano la kuwania ubingwa wa Shirikisho la Ngumi la Dunia (WBU) litakalofanyika kesho kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.


Katika mapambano ya siku hiyo yaliyoandaliwa na Hall Fame Boxing & Promotions yaliyopewa jina la'Usiku wa ubingwa Tanzania', Cheka ambaye ni bingwa wa Afrika wa IBF mwenye rekodi ya 28-7 KO 6, atavaana na mpinzani wake William kutoka Jimbo la Minneapolis, Minnesota Marekani mwenye rekodi ya 12-5 KO 11.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, mratibu wa pambano hilo kutoka kampuni ya Hall of Fame, Jay Msangi, alisema kuwa maandalizi yamekamilika kama walivyopanga ikiwa ni pamoja na kuwasili kwa mabondia kutoka Marekani.

Msangi alisema kuwa mabondia watapima uzito leo saa 3:00 asubuhi kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo).

Alisema kabla ya pambano kuu la kina Cheka kutakuwa pia na pambano jingine la raundi 12 kuwania mkanda wa Afrika uzito wa 'super middle' ambapo Mada Maugo (15-9, KO 11) aliye namba tatu kwa ubora nchini anatarajiwa kupambana na Thomas Mashali (8-1,KO 5),  wote wa hapa nchini.

Alisema vilevile kuwa kesho, Alphonce Mchumiatumbo (9-0, KO 8) atachuana na DeAndre 'Showtime' McCole kutoka Marekani katika pambano la raundi 10 huku Cosmas Cheka (8-3) akitwangana na Alan Kamote (20-6, KO 12) raundi sita.

Rais wa WBF, Howard Goldberg, alisema kuwa shirikisho lake limeamua kuyaleta mapambano hayo nchini kwa lengo la kukuza mchezo wa ngumi Tanzania na hiyo imetokana na kutambua vipaji vya mabondia wake.

"Hata kama Cheka atashinda, ni lazima aende Marekani kupambana tena na Phil... na atapanda tena jukwaani kucheza pambano lingine na bondia mwingine wa Marekani," alisema Goldberg.

Akizungumzia pambano hilo, William alisema mpinzani wake asitarajie kupata walau sare kwani yeye amekuja nchini kuendeleza rekodi yake ya kushinda.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa