Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIPA WA SIMBA APELEKWA JESHINI

KIPA namba moja wa Simba SC, Abbel Dhaira amekwenda kufanyiwa uchunguzi asubuhi hii katika hospitali Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kitengo cha wanamaji kutokana na matatizo ya msuli wa nyuma ya shingo.

Daktari wa Simba SC, Yassin Gembe amesema leo kwamba Dhaira amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya msuli wa nyuma ya shingo tangu kwenye mechi dhidi ya Yanga Jumapili ambayo alifungwa mabao matatu katika sare ya 3-3.
Abbel Dhaira

“Kama utakumbuka katika mechi dhidi ya Yanga alitibiwa tibiwa wakati mchezo unaendelea, ni kutokana na matatizo hayo hayo, kwa hivyo sasa hivi nakwenda naye akafanyiwe uchunguzi,”amesema Gembe asubuhi hii.

Dhaira alitoka dakika ya 35 juzi katika mchezo dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Mkwakwani, Tanga baada ya kugongana na mshambuliaji wa Coastal Union, Haruna Moshi ‘Boban’, timu hizo zikitoka sare ya 0-0.


Kipa huyo alisema alipata maumivu madogo kichwani, ambayo anaamini hayatamuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu na anataraia kucheza Jumatatu mechi nyingine ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Jumatatu dhidi ya Azam Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba SC imerejea Dar es Salaam jana na tayari ipo kambini kwake, Bamba Beach, Kigamboni ikiendelea na maandalizi ya mechi dhidi ya Azam.

Mechi hiyo inatarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na timu hizo kukabana kileleni, zote zikiwa na pointi 20 sawa na Mbeya City baada ya mechi 10, lakini Simba SC inaizidi Azam wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa