LEWANDOWSKI AISAMBARATISHA ARSENAL

BAO la dakika za lala salama la Robert Lewandowski limeipa ushindi wa 2-1 Borussia Dortmund dhidi ya Arsenal katika Ligi ya Mabingwa Uwanja wa Emirates usiku huu.

Henrikh Mkhitaryan aliifungia bao la kuongoza Borussia Dortmund, lakini Olivier Giroud akasawazisha ikawa 1-1.

Lakini katika dakika 10 za mwisho, Arsenal ikatepeta na kumruhusu mshambuliaji Lewandowski kuwamaliza nyumbani.


Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Ramsey, Arteta, Wilshere, Ozil, Rosicky na Giroud.

Borussia Dortmund: Weidenfeller, Grosskreutz, Subotic, Hummels, Schmelzer, Bender, Sahin, Blaszczykowski, Mkhitaryan, Reus na Lewandowski.

Katika mchezo mwingine, Chelsea imeshinda ugenini mabao 3-0 dhidi ya Schalke yaUjerumani, mabao ya Fernando Torres mawili na Eden Hazard moja.
Nayo AC Milan imelazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Barcelona katika mechi ya Ligi ya Mabingwa usiku huu Uwanja wa San Siro.

Robinho alitangulia kuwafungia wenyeji bao dakika ya tisa, pasi ya Mbrazil mwenzake, Kaka- lakini Lionel Messi akaisawazishia Barca dakika ya 24 kwa pasi ya Iniesta.

Mechi nyingine, Steaua Bucuresti imetoka 1 - 1 na
Basel, Olympique Marseille imefungwa 2-1 na Napoli, Porto imelala 1-0 mbele ya Zenit, Austria Wien imefungwa 3-0 na Atletico Madrid    na Celtic imeshinda 2 - 1 dhidi ya Ajax.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI