Ruka hadi kwenye maudhui makuu

'WAASI WA M23' WAIBUKIA SHEREHE DAR.

Hali si shwari hasa kwa wakazi wa maeneo ya Tabata na Kigogo jijini Dar es Salaam kufuatia kutokea kwa kikundi cha vijana wadogo wenye umri wa miaka 12-17 wanaojiita 'Waasi wa M23' kuvamia sherehe mbalimbali na kufanya vurugu huku wakiwa na silaha za jadi yakiwemo mapanga, visu na bisibisi.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na mtandao wa Mambo Uwanjani Leo ambao huko jirani na maeneo hayo umebaini kuwa kikundi cha vijana hao wanajitokeza nyakati za usiku kwenye sherehe za aina mbalimbali zinazohusisha muziki.


Vijana hao hufanya vurugu na uparaji ambapo mamia ya watu wamekuwa wakilalamika kuporwa mali zao ikiwemo simu na fedha, waathilika wakubwa ni akina mama ambao wamekuwa wahuzuliaji wakubwa katika sherehe hizo ambapo wameweza kulizwa na vijana hao.

Tayari vijana hao wameshafanya uasi wao na kuendelea kuwa tishio kwa wakazi waishio maeneo hayo na mengineyo jirani, kikundi hicho kilichokusanya vijana wenye kuhitajika na taifa kwa ajili ya masomo wamejikuta wakijiingiza kwenye uharifu huo, pia wanatumia dawa za kulevya ikiwemo bangi na mirungi.

Baadhi ya wakazi wa Tabata na Kigogo wamefanikiwa kuzungumxa na mtandao kwa kukata kutaja majina yao wamedai kuwa kikundi hicho ni hatari kwao kwani hutumia silaha za jadi na kuzuru watu, mbali zaidi jeshi la polisi limeshindwa kuwathibiti vijana hao hasa kutokana na kutofahamika vizuri.

Mkazi mwingine wa Tabata amelitaka jeshi la polisi kujitokeza mara wanapoombwa ili kuweza kuwabaini waharifu hao wanaochafua sura ya jiji la Dar es Salaam na nchi kwa ujumla, 'Kwanza wanajiita Waasi wa M23' ambao ni hatari kwetu' alisema mkazi mmoja wa Kigogo.

Kuwepo kwa kikundi hicho kunarudisha enzi za vikundi vya Komando Yosso na Kiboko ya Msheli vilivyokuwa tishio kwa wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa