Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HAMISI KIIZA AMGWAYA TAMBWE, UFUNGAJI BORA

Mshambuliaji  Mganda Hamis Kiiza wa Yanga amesema kuwa kwa sasa hawazii kiatu cha dhahabu cha mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu huu, bali mawazo yake yamejikita katika kuhakikisha anaisaidia timu yake kutetea ubingwa wa ligi hiyo.

Kiiza alisema baada ya mazoezi ya Yanga kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola uliopo Mabibo jijini Dar es Salaam jana kuwa hashindani na wachezaji wengine kusaka zawadi ya mfungaji bora bali anasaka mafanikio ya kikosi cha 'Wanajangwani'.


"Kikubwa ni kutetea ubingwa, zawadi ya mfungaji bora siifikirii sana kwa sasa. Naamini kufunga magoli mengi kutaisaidia timu yetu kuibuka bingwa tena. Na tukishakuwa na magoli mengi, kiatu cha dhababu kitakuja chenyewe, alisema Kiiza ambaye juzi alifunga goli moja na kufikisha magoli nane katika michezo saba ya ligi hiyo msimu huu.
Amemfikia aliyekuwa kinara pekee, Amisi Tambwe wa Simba.

Katika hatua nyingine, kiungo 'fundi' Haruna Niyonzima 'Fabregas' , aliyeukosa mchezo wa juzi walioshinda 3-0 dhidi ya Mgambo JKT kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kutokana na matatizo ya kifamilia, anatarajiwa kurejea mazoezini leo.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, kiungo huyo atarejea dimbani leo kujiandaa kwa mchezo wao wa kesho dhidi ya JKT Ruvu ya Pwani utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa baada ya kumalizika kwa siku tatu za ruhusa aliyoomba kwa ajili ya kumaliza matatizo ya kifamilia yaliyokuwa yanamkabili.

Niyonzima alirejea kwao Rwanda siku nne zilizopita na alitarajiwa kurudi jana kuungana na kikosi cha kocha Mholanzi Ernie Brandts.

Wachezaji wengine wa Yanga ambao walikosa mazoezi ya jana yaliyofanyika kwa saa mbili kuanzia saa 3:00 asubuhi kutokana na majeraha ni pamoja na kiungo Nizar Khalfan, beki wa pembeni Juma Abdul na kiungo Salum Telela.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa