MOYES AANZA NGEBE MAN UNITED IKIUA 4-0

MSHAMBULIAJI Javier Hernandez 'Chicharito' ameendeleza takwimu zake nzuri ndani ya Manchester United, licha ya kupewa nafasi chache za kucheza kwenye timu hiyo.

Nyota huyo wa Mexico usiku wa jana amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 wa Manchester United dhidi ya Norwich katika Kombe la Ligi.

Nyota huyo mwenye kipaji cha kufunga, alitikisa nyavu katika dakikaa 20 na 54 kwa penalti jana, wakati mabao mengine yalifungwa na Jones dakika ya 87 na Fabio dakika ya 90 na ushei.


Kikosi cha Man Utd jana kilikuwa: Lindegaard; Rafael, Ferdinand, Vidic, Büttner; Zaha/Rooney dk78, Cleverley/Anderson dk90, Jones, Young, Januzaj/Fabio dk90+3 na Hernandez.

Norwich: Bunn; Whittaker, R. Bennett, Bassong, Garrido; Snodgrass/Pilkington dk65, Fer, Johnson, Redmond/Murphy dk76, Hoolahan/Hooper dk89 na Elmander.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI