Kikosi cha Azam FC kimeondoka leo jijini Dar es Salaam kuelekea Singida kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Singida Black Stars.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Aprili Mosi, mwaka huu ambapo Azam FC itakuwa ikisaka alama muhimu katika mbio za ligi hiyo, huku Singida Black Stars nao wakilenga kutumia faida ya uwanja wa nyumbani.






