Duke Abuye ang' ara Harambee Stars, FIFA Series
Duke Abuya leo ameiongoza timu yake ya taifa ya Kenya kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Grenada katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu wa mashindano ya FIFA series.
Duke alianza kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo kabla ya baadae kuja kufanyiwa mabadiliko kwenye dakika ya 78.
Mohamed Bajaber nae alikuwepo kwenye mchezo huo, yeye aliingia mwanzoni mwa kipindi cha pili na akacheza dakika zote 45+5 za kipindi cha pili.
