CAF yaanza kumeguka, Veron aachia ngazi

Veron Mosengo-Omba amestaafu rasmi kama Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka barani Afrika CAF.

Sura muhimu inafungwa katika katika shirikisho la soka Afrika CAF ambapo Mosengo-Omba alikuwa na jukumu muhimu katika usimamizi na mageuzi ya kandanda ya Afrika.

Kwasasa nguvu anazielekeza katika majukumu mengine ya kisoka akiwa miongoni mwa wagombea wa Rais wa shirikisho la soka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Uchaguzi ambao ungefanyika mwezi huu ulisogezwa mbele baada ya FIFA kubaini uwepo wa uhaba wa fedha za kuandaa uchaguzi huo.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI