Depu aanza mazoezi Yanga, sasa mabeki watamkoma
MSHAMBULIAJI wa Yanga, raia wa Angola, Laurindo Dilson Maria Aurélio ‘Depu’ aliyekuwa anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja leo ameanza mazoezi mepesi ya peke yake.
Depu alikuwa akijifua peke yake leo Yanga ikijiandaa na mchezo ujao wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara dhidi ya Tanzania Prisons Aprili 4 Uwanja wa KMC Complex, Mwenge, Dar es Salaam
