Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2025

Simba yaendelea kugawa pointi Ligi ya mabingwa Afrika

TIMU ya Simba SC imepoteza mechi ya pili mfululizo ya Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1 na wenyeji, Stade Malien usiku huu Uwanja wa Machi 26 Jijini Bamako nchini Mali. Mabao ya Stade Malien yamefungwa na mshambuliaji Mcameroon, Taddeus Nkeng dakika ya 16 na beki mzawa, Ismaila Simpara dakika ya 23, wakati bao pekee la Simba limefungwa na kiungo wa Afrika Kusini, Neo Maema dakika ya 54. Kipa wa Simba SC, Yakoub Suleiman Ali alipangua mkwaju wa penalti wa Mcameroon Taddeus Nkeng dakika ya 62, kabla ya kiungo Msenegal wa Wekundu hao wa Msimbazi, Alassane Kante kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 82. Kwa ushindi huo, Stade Malien inafikisha pointi nne sawa na Petro de Luanda ya Angola timu hizo zikilingana hadi wastani wa mabao baada ya mechi za mwanzo, zikifuatiwa na Espérance de Tunis yenye pointi mbili na Simba SC inaendelea kushika mkia baada ya kupoteza mechi zote mbili za mwanzo. Ikumbukwe mechi ya kwanza Simba SC ilifungwa 1-0 na Petro de Luanda ya Angol...

Serikali yakwepa mabadiliko Simba

SERIKALI imesisitiza kuwa haitalazimisha Klabu yoyote nchini kufanya mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji bila uamuzi wa wanachama wake, na kwamba jukumu lake kuu ni kuhakikisha mchakato wowote unaotekelezwa unaendana na Sheria za nchi pamoja na kanuni zinazoongoza mchezo wa mpira wa miguu. Kauli hiyo imetolewa leo, Novemba 30, 2025, na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’ wakati akihutubia Mkutano Mkuu wa mwaka wa Klabu ya Simba uliofanyika jijini Dar es Salaam. Mhe. Mwinjuma amesema kuwa, hatima ya mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji wa klabu hiyo iko mikononi mwa wanachama, na Serikali haina dhamira ya kuingilia maamuzi yao. “Mchakato huu ni wenu; ni uamuzi wa wanachama. Kama mtakubaliana kuendelea, kutathmini upya au kubadili mwelekeo, basi uamuzi huo utaheshimiwa,” amesema Mhe. Mwinjuma. Ameongeza kuwa, Serikali inatamani kuona mijadala na maamuzi kuhusu mustakabali wa klabu hiyo haitawaliwi na hisia bali busara, kuzingatia sheria, maslahi...

Mbeya City yafurusha makocha wake wote

TIMU ya Mbeya City imefukuza makocha wake wote baada ya kufungwa 1-0 na Namungo FC leo katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.

Mbwana Samatta hajafunga wala kutoa assist Ufaransa

Hali si shwari kabisa huko Ufaransa kwa mshambuliaji wa taifa la Tanzania na klabu yake ya Le Havre Mbwana Ally Samatta. Samatta alisajiliwa na klabu ya Le Havre kama mchezaji huru August 5 mwaka huu baada ya mkataba wake na klabu ya Paok ya Ugiriki kutamatika. Mpaka kufikia sasa Samatta hajafanikiwa kufunga bao hata moja wala kutoa pasi ya bao licha ya kuanza kwenye miche 8 kati 13 ya ligi ambayo klabu ya Le Havre imeshacheza. Kwa sasa klabu ya Le Havre inashika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi kuu baada kucheza za michezo 13,kushinda michezo 3,sare 5 na vipigo 5.

Eto' o achaguliwa tena urais Cameroon

Mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Barcelona na Vilabu vingine mbalimbali ulimwenguni Samuel Eto’o Fils (44), amechaguliwa kuwa Rais wa Shirikisho la Soka Cameroon (FECAFOOT) kwa mara ya pili mfululizo. Katika Mkutano wa Uchaguzi mkuu uliofanyika huko Mbankomo eneo la kati la Cameroon karibu na mji mkuu wa YaoundĂ©,amechaguliwa kwa kura 85 kati 87 ambapo kura mbili zimeharibika. Eto’o alichaguliwa kwa mara ya kwanza kuongoza FECAFOOT mnamo Desemba 2021. Mchakato wa Uchaguzi umekabiliwa na mvutano wa kisiasa huku Wizara ya Michezo ikijaribu kusimamisha Uchaguzi huo hapo awali lakini FECAFOOT ukasisitiza kwamba taratibu zake zinafuata kanuni za Kimataifa za Mpira wa Miguu. Wagombea wengine wawili Yianick Heumo Leudjeu na Georges Kalgong waliondolewa kwenye mchakato huo na kumuacha Eto’o akiwa Mgombea pekee.

Amani Kyata kocha mpya wa viungo Namungo FC

Amani Kyata amejiunga na klabu ya Namungo FC akiwa ndiye kocha wa viungo na Utimamu wa Mwili wa wachezaji lakini pia ndiye opposition analyst wa wauaji hao wa Kusini kwenye ligi kuu. Kyata amewahi kuhudumu kama kocha wa viungo msimu uliopita akiwa na Kagera Sugar kabla ya kujiunga na Namungo pia ni kocha mwenye Fitness Licence na CAF C Diploma

Yanga ni TP Mazembe mpya ya barani Afrika

Anaandika Shafih Dauda KABLA ya klabu za Tanzania kuingia kwenye ramani za soka la Ushindani wa kiwango cha juu barani Afrika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati Timu ya mfano ilikuwa ni TP Mazembe ya Congo DR . TP Mazembe alikuwa kawaida sana kwake kuifunga timu yoyote ile Afrika , Kawaida kufika hatua za juu na hata kushinda Taji la Afrika kiasi cha kuvutia wachezaji wengi wenye uwezo kutamani kuitumikia hii ni kutoka na namna walivyoijenga project yao. Miaka imekimbia project ya Mazembe imefika ukomo na sasa Mazembe haipo tena kwenye hiyo nafasi , na sisi Tanzania kwa sasa ndio tumelishika soka la Afrika Mashariki na Kati kwenye kila kitu Binafsi yangu Naitazama Yanga SC kama timu iliyorithi mazuri ya TP Mazembe na kuongeza mengine makubwa kiasi cha wao kwa sasa kuwa ndio timu bora ya mfano na tishio zaidi kwa ukanda wetu. Project ya Yanga ambayo kwa sasa imefikisha miaka 4 , imeleta Fainali ya Shirikisho , Robo Fainali Klabu bingwa , Makundi Back to Back , Makombe ya Ndani back to b...

TRA United yageuzwa nyanya na Mtibwa Sugar

Timu ya Mtibwa Sugar ya Manungu mkoani Morogoro imeifunga TRA United mabao 2-1 mchezo wa Ligi Kuu bara. Mabao ya Mtibwa Sugar inayonolewa na Yusuph Chipo yamefungwa na Kassim Shaibu dakika ya 40 na Ismailia Mjesa dakika ya 90 wakati bao la kufutia machozi la TRA United limefungwa na Adam Adam dakika ya 13

Aziz Ki hali tete kiafya

Mchezaji wa Wydad Athletic Club Stephanie Aziz Ki siku ya Jana alipata jeraha lililompelekea kuhusu maumivu makali ya kichwa na kufabya awahishwe hospital Kwa ajili ya matibabu ya dharula. Idara ya matabibu wa Wydad Athletic Club imetoa taarifa kuwa mchezaji huyo bado anaendelea kupatiwa matibabu Zanzibar.

Pamba Jiji yazamisha jahazi la KMC

WENYEJI, Pamba Jiji FC wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya KMC FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya Uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza. Mabao yote ya ‘Wana Kawekamo’ jioni leo yamefungwa na mshambuliaji Mkenya - Mathew Tegisi Momanyi dakika ya saba na 26 na kwa ushindi huo – Pamba Jiji inafikisha pointi 15 na kupanda tena kileleni, wakiizidi pointi mbili JKT Tanzania baada ya wote kucheza mechi nane. Kwa upande wao, KMC hali inazidi kuwa mbaya baada ya kupoteza mchezo wa sita leo, wakiwa wametoa sare moja na kushinda moja kati ya nane walizocheza, hivyo wanabaki na pointi zao nne wakiendelea kushika mkia katika ligi ya timu 16.

Nassoro Idrissa amgaragaza Hosea na kuwa bosi wa Ligi Kuu

Nassoro Idrissa ameshinda nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi ya Tanzania baada ya Kumshinda Hosea Lugano kwa Kura 7 kwa 6 Nassoro Idrissa ni Rais wa Azam FC, kabla ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Ligi, alikuwa akikaimu nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Almas Kasongp. Nassoro Idrissa

Al Ahly yaishusha Yanga kileleni

Al Ahly imerejea kileleni mwa Kundi B kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya wenyeji, AS Far Rabat, wakifikisha alama 4 baada ya mechi mbili sawa na Young Africans Sc iliyoshuka mpaka nafasi ya pili. AS FAR Rabat iliyopoteza 1-0 kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Wananchi ipo nafasi ya tatu alama moja baada ya mechi mbili huku JS Kablie iliyopoteza 4-1 dhidi ya Al Ahly kwenye mechi ya kwanza ikiburuza mkia alama moja baada ya mechi mbili. Kwingineko Mamelodi Sundowns imetoshana nguvu na MC Alger ya Algeria kwa sare tasa huku Sundowns ikikwea kileleni mwa Kundi C alama nne baada ya mechi mbili huku MC Alger ikiwa nafasi ya tatu alama moja baada ya mechi mbili.

Yanga yapaa kileleni Ligi ya mabingwa

Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika, Yanga SC usiku huu imeilazimisha sare ya bila kufungana 0-0, wenyeji JS Kabylie ya Algeria na kufanikiwa kuongoza kundi B. Yanga SC ambao katika mchezo wake wa kwanza uliofanyika uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar dhidi ya FAR Rabat na kushinda 1-0, imecheza vizuri na kuondoka na pointi moja ugenini. Watani zao Simba SC wataingia dimbani keshokutwa itakapocheza na Stade Malien ya Mali mchezo utakaopigwa mjini Bamako, nchini Mali.

Balozi wa Tanzania nchini Mali, aitembelea Simba SC

Balozi wa Tanzania nchini Mali ambaye makazi yake yapo Abuja, Nigeria, Selestine Gervas Kakele, ametembelea mazoezi ya Simba SC, leo Novemba 28, uwanja wa Lafia Club De Bamako, mjini Bamako kwa ajili ya kuwapa hamasa kuelekea mchezo wa Jumapili wa kundi “D” Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Stade Malien. Balozi Kakele amewatia moyo wachezaji na kuwasisitiza kwamba, mchezo wa kwanza waliopoteza nyumbani dhidi ya Petro Atletico ya Angola ulishapita, sasa vita ni dhidi ya Stade Malien na imani yake timu itapata ushindi. Simba ipo Mali kucheza mchezo wake wa pili wa hatua ya makundi dhidi ya Stade Malien Jumapili ya Novemba 30, saa 1:00 usiku

Azam FC yaendelea kugawa pointi kombe la Shirikisho

Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC, usiku huu imepoteza mchezo mwingine baada ya kufungwa bao 1-0 na timu ya Wydad Athletic ya Morocco uwanja wa New Amaan Stadium Zanzibar. Bao pekee la Wydad Athletic limefungwa na Nordin Amrabat dakika ya 56, huu ni mchezo wa pili kwa Azam FC kupoteza baada ya kufungwa mabao 2-0 katika mchezo wake wa kwanza uliofanyika ugenini.

Mashujaa FC na Dodoma Jiji mwendo wa sare sare maua

WENYEJI, Mashujaa FC wamelazimishwa sare ya bila mabao na Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma. Kwa matokeo hayo, Mashujaa FC wanafikisha pointi 12 na kusogea nafasi ya tatu wakizidiwa pointi moja na JKT Tanzania baada ya wote kucheza mechi nane — wakati Pamba Jiji FC pia ina pointi 12, lakini imecheza mechi saba. Kwa upande wao Dodoma Jiji FC baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao sita za mechi nane sasa nafasi ya 14 kwenye Ligi ya timu 16.

Mousa Camara amaliza matibabu yake Morocco

KIPA namba moja wa Simba SC, Mousa ‘Pin Pin’ Camara raia wa Guinea alikamilisha matibabu yake ya upasuaji wa goti nchini Morocco na sasa anatarajiwa kurejea nchini kwa mapumziko ya wiki 10. Camara aliyeondoka nchini Novemba 17, aliumia dakika ya 77 kwenye mchezo wa marudiano wa Raundi ya Pili Ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United ya Botswana Septemba 28 mwaka huu Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam timu hizo zikitoka sare ya 1-1. Simba ikafanikiwa kusonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 2-1 kufuatia kushinda 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Septemba 20 Uwanja wa Taifa wa Botswana Jijini Gaborone. Katika Raundi ya pili Simba iliitoa pia Nsingizini Hotspurs ya Eswatini kwa ushindi wan ugenini wa 3-0 Oktoba 19 Uwanja wa Taifa wa Somhlolo mjini Lobamba na sare ya bila mabao Oktkba 26 Uwanja wa Mkapa na kuingia hatua ya makundi, ambako wamepangwa Kundi D pamoja na EspĂ©rance de Tunis ya Tunisia, Petro de Luanda ya Angola na Stade Malien ya Mali. Ni kipa mpya aliyesajiliwa kutoka JKT ...

Winga Al Hilal Omduman afungiwa mechi 3

Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) imemfungia mechi tatu na kumtoza faini ya dola za Kimarekanl 5,000 (sawa ba zaidi ya Milioni 12 za Kitanzania) winga wa klabu ya Al Hilal Omduman ya Sudan Girumugish kwa vitendo visivyo vya kiungwana michezoni kutokana na alichokifanya baada ya mchezo wa timu yake na Mc Alger uliopigwa Novemba 28 na kumalizika kwa Al hilal kiushinda bo 2-1. Kutokana na adhabu hiyo, Girumugisha ataikosa michezo hii: • vs St Eloi Lupopo • vs Mamelodi Sundowns • vs Mamelodi Sundowns Caf waneweka wazi madai ya nyota huyo kurusha chupa kwenye benchi la Mc Alger sio miongoni mwa vitendo vilivyoainishwa kama ilivyokuwa ikieleza awali.

Andy Boyeli kutupiwa virago Yanga

Inasemekana klabu ya Yanga SC inaweza kuachana na mshambuliaji wake Andy Boyeli raia wa DR Congo baada ya kushindwa kuonesha kiwango chake. Boyeli alisajiliwa kwa mkopo kutoka kwenye klabu ya Shenkhume United ya Afrika Kusini na tayari Yanga wameshaijulisha klabu hiyo mpango wa kumuacha. Wanajangwani hao watasajili mshambuliaji mpya katika dirisha dogo la Januari.

Wekundu ndani ya Bamako, Mali

Wachezaji wa kikosi cha Simba SC tayari wameshawasili mjini Bamako nchini Mali kwa ajili ya mchezo wa pili wa Ligi ya mabingwa Afrika mwishoni mwa wiki hii. Pichani ni baadhi ya wachezaji wakitua Bamako.

Baadhi ya viongozi wa Simba wana afya ya akili - Magori

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba SC Crescentius Magori amesema kuna baadhi ya viongozi wa tatizo la afya ya akili wanafurahi hadi timu ikifungwa, kazi yao nikuleta taharuki, hawataki utulivu kwenye klabu Magori anawaita wanachama wajitokeze kwenye mkutano mkuu November 30

Pedro akiri JS Kabyile ni wapinzani wagumu sana

Ni mchezo wa pili katika hili kundi gumu zaidi, tumefanikiwa kupata pointi 3 za kwanza nyumbani na kesho tuna mechi nyingine ngumu hapa dhidi ya JS Kabylie. “Ni mpinzani mgumu sana na ana nguvu kubwa ya mashabiki. Hii ni mara yangu ya nne nakuja hapa Algeria kuwaona JS Kabilie. Ni Klabu yenye hamasa na mashabiki wengi sana” “Kwetu Yanga ni mazingira mazuri kuwepo hapa, kucheza dhidi ya Klabu mbele mbele ya mashabiki wengi pia uwanjani, tumekuja kupambana kupata pointi 3 hapa na sio kitu kingine.”

Logo ya Simba yapingwa na ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali

Kwa mujibu wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Logo ya Simba Sports Club haitambuliki kisheria hii ambayo inatumika sasa maana ni tofauti na iliyosajiliwa, Ofisi ya AG inashauri Klabu isajili logo ya sasa maana Mtu akiitumia vinginevyo hakuna uhalali wa kumtia hatiani kisheria itakuwa ngumu na klabu inaweza kupoteza haki zake. Yaani kiufundi Mtu akitumia logo ya sasa kuzalisha chochote sio kosa maana haipo kisheria. Hata Logo zilizosajiliwa zilitakiwa kuwa zimehuishwa kabla ya tarehe 4 Novemba, 2017. Inashauriwa Alama hizo zihuishwe ili kuondokana na hatari ya kufutwa kutoka katika Rejista ya Msajili wa Alama za Biashara na Huduma(BRELA) kwa mujibu wa Kanuni ya 54 – 55 ya Kanuni za Alama za Biashara na Huduma za Mwaka 2000.

Serikali inamtambua Murtaza Mangungu kama mwenyekiti wa Bodi, Simba SC na sio Magori

Serikali kupitia Baraza la michezo imetoa maelekezo Katiba mpya ya Simba SC inapaswa kumtambua M/Kiti wa Klabu kuwa ndiye M/Kiti wa Bodi ya Wakurugenzi maana klabu ina umiliki mkubwa ( 51%) na wawekezaji (49%). Serikali inataka kuwe na wawekezaji kuanzia watatu. Serikali imetaka Katiba ifanyiwe maboresho ya kutamka bayana kuwa Mwenyekiti wa Simba Sports Club ndiye Kiongozi Mkuu wa Chombo cha Utawala ndani ya Klabu na hivyo awe na mamlaka ya kuitisha mkutano mkuu wa wanachama kwa kuwa masuala yanayojadiliwa juu ya uanachama na maendeleo ya Klabu yanaathiri moja kwa moja maslahi ya wanachama. Mwenyekiti wa Klabu huyo ndiye awe Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Sports Club Company Limited kwa kuzingatia kuwa wanachama kupitia Klabu ndio wenye umiliki wa hisa nyingi (51%) na hivyo viongozi wote walio chini ya Katiba ya Klabu watawajibika kwake katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, Katiba na kanuni zinazoongoza Klabu. Serikali pia imetaka kurekebishwa kwa matumizi y...

DIMITAR PANTEV NI BONGE LA KOCHA, WASIOJUA MPIRA WANAMWADHIBU

Na Prince Hoza Matua TANGU msimu wa 2025/2026 wa michuano ya CAF ilipoanza na Simba SC kupata nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya mabingwa barani Afrika na kwa jitihada zake ikafanikiwa kutinga hatua ya makundi. Haikuwa rahisi Simba SC ilianzia raundi ya awali na ilipangwa kukutana na klabu ya Gaborone United ya Botswana ambapo ilianzia ugenini, Wekundu wa Msimbazi, walisafiri hadi mjini Gaborone na kukutana na miamba hiyo ya Gaborone United. Simba ilikuwa ikinolewa na kocha wake Fadlu David's raia wa Afrika Kusini na iliingia kwenye mchezo huo huku kukiwa na tetesi kwamba kocha wake mkuu Fadlu anataka kubwaga manyanga. Na ilidaiwa kwamba kocha huyo ataaga baada ya mchezo huo, kuna mambo mengi yameibuka ndani ya klabu hiyo ingawa tulijua kama tetesi tu yanasemwa mchana na usiku watalala, lakini Simba katika mchezo huo iliibuka na ushindi wa bao 1-0. Baadaye Fadlu alibwaga manyanga na kutimkia klabu yake ya zamani ya Raja Athletic Club ya Morocco, ikabidi Simba irejee Dar es Sal...

Meneja Simba awahofii Stade Malien

"Stade Malien walivuna alama moja lakini Esperance walikuwa bora zaidi kwenye mchezo baina yao, na walipoteza nafasi nyingi sana hivyo nadhani Esperance wana ubora wa juu kuliko Malien. Malien wana wachezaji wazuri, lakini mara nyingi wanahusudu matumizi makubwa na kucheza soka la kushambulia moja kwa moja (direct football), hivyo nadhani tuna nafasi. Sisi tuna timu bora zaidi na tuna wachezaji bora ukilinganisha na Stade Malien, tuna wachezaji wazuri kwenye kila eneo Nadhani kwetu sio changamoto kwenda kucheza kwao, kwa sababu uwanja wao una sehemu kubwa ya kuchezea na mzuri hivyo tunaweza kucheza aina yetu ya soka. Na tunachohitaji ni kufunga tu.." -Dimitarantev, Meneja wa Simba SC

Simba wapaa kwenda Bamako kuifuata Stade Malien

KIKOSI cha Simba SC kimeondoka Alfajiri ya leo kwenda Mali kwa ajili ya mchezo wake wa pili wa Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji, Stade Malien ya Mali Jumapili ya Novemba 30 Uwanja wa Machi 26 Jijini Bamako. Simba SC imeondoka na kikosi cha wachezaji 21 kwa ajili ya mchezo huo wa ugenini, wakiwemo makipa wawili — Yakoub Suleiman Ali na Hussein Abel. Simba inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kufufua matumaini ya kwenda Robo Fainali baada ya Jumapili Simba SC kuanza vibaya hatua ya makundi ya michuano hiyo ikifungwa 1-0 na Petro de Luanda ya Angola Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam. Bao pekee lililoizamisha Simba SC lilifungwa na kiungo Mreno, Bernardo Oliveira Dias dakika ya 78 alipofumua shuti la umbali wa Nita 20 ambalo lilimbabatiza beki raia wa Afrika Kusini, Rushine De Reuck na kubadili njia likimpoteza mwelekeo kipa namba moja Tanzania, Yakoub Suleiman Ali. Mechi nyingine ya Kundi D Jumapili EspĂ©rance ililazimishwa sare ya bila mabao na Stade Malien ...