Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Serikali inamtambua Murtaza Mangungu kama mwenyekiti wa Bodi, Simba SC na sio Magori

Serikali kupitia Baraza la michezo imetoa maelekezo Katiba mpya ya Simba SC inapaswa kumtambua M/Kiti wa Klabu kuwa ndiye M/Kiti wa Bodi ya Wakurugenzi maana klabu ina umiliki mkubwa ( 51%) na wawekezaji (49%).

Serikali inataka kuwe na wawekezaji kuanzia watatu.

Serikali imetaka Katiba ifanyiwe maboresho ya kutamka bayana kuwa Mwenyekiti wa Simba Sports Club ndiye Kiongozi Mkuu wa Chombo cha Utawala ndani ya Klabu na hivyo awe na mamlaka ya kuitisha mkutano mkuu wa wanachama kwa kuwa masuala yanayojadiliwa juu ya uanachama na maendeleo ya Klabu yanaathiri moja kwa moja maslahi ya wanachama.

Mwenyekiti wa Klabu huyo ndiye awe Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba Sports Club Company Limited kwa kuzingatia kuwa wanachama kupitia Klabu ndio wenye umiliki wa hisa nyingi (51%) na hivyo viongozi wote walio chini ya Katiba ya Klabu watawajibika kwake katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria, Katiba na kanuni zinazoongoza Klabu.

Serikali pia imetaka kurekebishwa kwa matumizi ya neno "MWEKEZAJI" ndani ya rasimu ya Katiba na badala yake itumike dhana pana ya "WAWEKEZAJI" na iweke bayana kuwa Baraza la Wadhamini kwa niaba ya wanachama, ndilo litakaloingia mikataba na makubaliano yoyote na wawekezaji.

Marekebisho haya yanakusudia kupanua wigo wa uwekezaji wa kibiashara ndani ya Klabu kwa maendeleo ya Klabu na ulinzi wa maslahi ya wanachama kama wamiliki halali wa Simba Sports Club.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa