Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba yaendelea kugawa pointi Ligi ya mabingwa Afrika

TIMU ya Simba SC imepoteza mechi ya pili mfululizo ya Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kufungwa mabao 2-1 na wenyeji, Stade Malien usiku huu Uwanja wa Machi 26 Jijini Bamako nchini Mali.

Mabao ya Stade Malien yamefungwa na mshambuliaji Mcameroon, Taddeus Nkeng dakika ya 16 na beki mzawa, Ismaila Simpara dakika ya 23, wakati bao pekee la Simba limefungwa na kiungo wa Afrika Kusini, Neo Maema dakika ya 54.

Kipa wa Simba SC, Yakoub Suleiman Ali alipangua mkwaju wa penalti wa Mcameroon Taddeus Nkeng dakika ya 62, kabla ya kiungo Msenegal wa Wekundu hao wa Msimbazi, Alassane Kante kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 82.

Kwa ushindi huo, Stade Malien inafikisha pointi nne sawa na Petro de Luanda ya Angola timu hizo zikilingana hadi wastani wa mabao baada ya mechi za mwanzo, zikifuatiwa na Espérance de Tunis yenye pointi mbili na Simba SC inaendelea kushika mkia baada ya kupoteza mechi zote mbili za mwanzo.

Ikumbukwe mechi ya kwanza Simba SC ilifungwa 1-0 na Petro de Luanda ya Angola Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, wakati Stade Malien ililazimishwa sare ya bila mabao na Espérance Uwanja wa Hammadi Agrebi, Tunisde Jijini Tunis nchini Tunisia.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa