Ruka hadi kwenye maudhui makuu

DIMITAR PANTEV NI BONGE LA KOCHA, WASIOJUA MPIRA WANAMWADHIBU

Na Prince Hoza Matua

TANGU msimu wa 2025/2026 wa michuano ya CAF ilipoanza na Simba SC kupata nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya mabingwa barani Afrika na kwa jitihada zake ikafanikiwa kutinga hatua ya makundi.

Haikuwa rahisi Simba SC ilianzia raundi ya awali na ilipangwa kukutana na klabu ya Gaborone United ya Botswana ambapo ilianzia ugenini, Wekundu wa Msimbazi, walisafiri hadi mjini Gaborone na kukutana na miamba hiyo ya Gaborone United.

Simba ilikuwa ikinolewa na kocha wake Fadlu David's raia wa Afrika Kusini na iliingia kwenye mchezo huo huku kukiwa na tetesi kwamba kocha wake mkuu Fadlu anataka kubwaga manyanga.

Na ilidaiwa kwamba kocha huyo ataaga baada ya mchezo huo, kuna mambo mengi yameibuka ndani ya klabu hiyo ingawa tulijua kama tetesi tu yanasemwa mchana na usiku watalala, lakini Simba katika mchezo huo iliibuka na ushindi wa bao 1-0.

Baadaye Fadlu alibwaga manyanga na kutimkia klabu yake ya zamani ya Raja Athletic Club ya Morocco, ikabidi Simba irejee Dar es Salaam bila kocha wake mkuu kwani hata kocha msaidizi Seleman Matola naye alikumbwa na adhabu.

Katika mchezo dhidi ya Gaborone United, Matola alioneshwa kadi nyekundu hivyo alishindwa kusimama kwenye mchezo wa marudiano jijini Dar es Salaam, uongozi wa Simba ilibidi ufanye mazungumzo na kocha wa timu ya taifa, Taifa Stars, Hemed Morocco Ili asimame katika touch line kwenye mchezo dhidi ya Gaborone United.

Morocco licha ya kuwa kocha wa Taifa Stars, lakini alienda kuisaidia Simba na kuiongoza katika mchezo huo wa marudiano dhidi ya Gaborone United na Simba kutinga hatua ya makundi baada ya sare ya kufungana bao 1-1.

Hata hivyo makubaliano ya Simba na Morocco yalikuwa ya mechi moja na Simba ilianza mchakato wa kutafuta kocha mpya, Dimitar Pantev raia wa Burgalia aliajiriwa na Simba kuwa kocha mkuu.

Leseni yake ya UEFA ilimfanya awe meneja mkuu badala ya kocha mkuu pale Simba inapocheza mechi za ligi za nyumbani lakini anakuwa kocha mkuu kwenye mechi za CAF.

Simba waliridhishwa na aina ya ufundishaji wake akiwa na klabu ya Gaborone United ambapo Simba ilipata tabu sana kuitoa timu hiyo kwenye mchezo wake wa raundi ya awali zilipokutana, Pantev ni kocha mwenye mikakati mikubwa na soka lake ni la kuvutia.

Mashabiki wa Simba wenyewe walifurahishwa na ujio wake, ni mburudishaji mzuri akiwa na timu yake ndani ya uwanja, na pia ana mbinu za kupata mabao, alianza mchezo wake dhidi ya Nsingizini Hotspurs ambapo Simba ilicheza ugenini na ikishinda mabao 3-0.

Anapendelea sana kutumia mshambuliaji kizuri yaani namba tisa wa uongo, alianza na Kibu Denis dhidi ya Nsingizini Hotspurs na Simba ikishinda 3-0 ambapo Kibu alifunga mabao mawili, na moja alifunga beki wa kati Wilson Nangu.

Simba imeanza kubadilika na mwenendo wake umekuwa mzuri ingawa msimu huu haijaweza kupata ushindi katika uwanja wa Mkapa, ikiwa chini ya Morocco Simba ilipata sare na Gaborone United 1-1 na chini ya Pantev ikapata sare ya 0-0 na Nsingizini Hotspurs.

Kufungwa 1-0 dhidi ya Petro de Luanda ya Angola hatua ya makundi zilipeleka lawama za wazi wazi kwa Pantev na akionekana si lolote si chochote, Pantev anaonekana si kocha kwa sababu hajamwazisha mshambuliaji halisi anayesimama mbele.

Kocha huyo amemtumia Elie Mpanzu kama mshambuliaji kivuli, mashabiki wa Simba wamemkataa na pia kila mmoja amegeuka mchambuzi akimkataa zaidi, kiukweli mimi binafsi nasema ni bonge la kocha kwani kuna kitu nakiona ndani ya Simba.

Kama akiendelea kuinoa timu hiyo ninaamini itakuwa timu tishio barani Afrika, licha kwamba amekuta wachezaji ambao sio bora sana, lakini ataibadili na kuijenga na hatimaye itakuwa timu tishio.

ALAMSIKI


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa