Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2026

Namungo FC yaidhibu KMC 1-0

WENYEJI, Namungo FC wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya KMC FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi. Pongezi kwq mfungaji wa bao hilo pekee, mshambuliani Mkongo Fabrice Ngoy wa Ngoy dakika ya 72 kwa penalti. Kwa ushindi huo, Namungo FC inafikisha pointi 18 katika mchezo wa 10 na kuruka juu kutoka nafasi ya saba hadi ya tatu, wakati KMC inayobaki na pointi zake tano za mechi 12 sasa inaendelea kushika mkia kwenye ligi ya timu 16.

Emam Ashour aomba radhi

Mchezaji wa Al Ahly Emam Ashour ameomba radhi kwa klabu ya Al Ahly kupitia kwa Meneja wa timu Walid Salah Eldin na kusema hakukusudia kukwazana na mtu yoyote na anaomba radhi akiomba arudishwe kikosini. Bado klabu haijatoa msimamo wake rasmi na wanasubiri kumaliza mechi ya Yanga kwanza ndio watakaa naye chini kuamua cha kufanya.

Simba waipashia Esperance kwa Mkapa

Wachezaji wa timu ya Simba SC ambayo kesho jioni itashuka uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam kumemyana na Esperance ya Tunisia mchezo wa Ligi ya mabingwa Afrika. Wachezaji wa timu hiyo walionekana wakifanya mazoezi kwa bidii wakisimamiwa na makocha wao wakiongozwa na mkuu Steve Barker. Kwa vyovyote tusubirie soka litakalotolewa na wachezaji hao ambao wameonekana kuwa na morali ya hali ya juu na kupania mchezo huo wakitaka ushindi wa kwanza.

Mabululu avunja mkataba kwa Waarabu ili atambulishwe Simba au Yanga

Klabu ya Al ahly Tripoli Ya Libya Imevunja mkataba na mshambuliaji wake Raia wa Angola Mabululu(33). Mchezaji huyo alietumika hapo Kwa msimu Mmoja na nusu kutokea Petro Athletico de Luanda ya nchini kwao Angola Sasa ni free agent. Dilisha la Usajili la Tanzania litafungwa Leo Tar31/1/2025. Muda nadhani unatunyima kuona jambo kubwa kwenye dilisha hili.

Yanga yabanwa na Al Ahly nyumbani

TIMU ya Yanga SC imelazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Al Ahly ya Misri katika mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Afrika jioni ya leo Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar. Yanga walitangulia kwa bao la beki wao wa kati, Ibrahim Hamad Abdullah ‘Bacca’ dakika ya 45’+1, kabla ya kiungo Aliou Dieng kuisawazishia Al Ahly dakika ya 60 akimchambua mchezaji mwenzake wa Mali, kipa Djigui Diarra. Kwa matokeo hayo, Yanga SC inafikisha pointi tano katika mchezo wa nne, ingawa inabaki nafasi ya pili ikizidiwa pointi tatu na Ahly wanaoongoza baada ya wote kucheza mechi nne. Mechi nyingine ya Kundi B itafuatia Saa 2:00 usiku Uwanja wa Prince Moulay Abdellah Jijini Rabat nchini Morocco — wenyeji, AS FAR Rabat wakimenyana na JS Kabylie ya Algeria. Kuelekea mchezo huo, zote AS FAR Rabat na JS Kabylie kila moja ina pointi mbili baada ya mechi tatu za awali zikifuatana nafasi ya tatu na ya nne. Ikumbukwe mechi zilizopita Yanga ilichapwa 2-0 na Al Ahly Uwanja wa Borg El Arab Jijini Alexandria na AS F...

Inspector Haroun: Muasisi wa jina la Wekundu wa Msimbazi kwa Simba SC

Harouna Kahena maarufu kama Inspector Haroun a k a Babu msanii wa muziki wa kizazi kipya anayeunda kundi la Gangwe Mob ambapo miaka ya 2001 lilitamba sana kwa nyimbo zake za Mtoto wa Geti kali na nyinginezo. Inspector Haroun ndiye aliyeasisi jina la Wekundu wa Msimbazi ambapo klabu ya Simba SC yenye maskani yake mtaa wa Msimbazi ikaamua ilitumie kuwa na miongoni mwa majina yake ya utani. Jina hilo, Inspector Haroun aliliimba katika wimbo wake uitwao 'Yanini bye bye " alioutoa mwaka 2002, na kuanzia hapo Simba SC ikaamua kujiita Wekundu wa Msimbazi. Inspector Haroun aliamua kuiita noti ya elfu kumi, (10,000) iliyokuwa ya rangi ya bluu ambapo wakati huo msanii Mr Blue alijitokeza kutokana na noti hiyo, Harouna yeye akaiita elfu kumi mpya yenye rangi nyekundu ambapo akaiita wekundu wa Msimbazi, akisema "Na sasa sio bluu bluu tena ni wekundu wa Msimbazi ", na hapo ndipo Simba walipopata fulsa ya kujiita Wekundu wa Msimbazi. KWAHIYO INSPECTOR HAROUN NDIYO MUASISI WA JINA ...

Balla Conte ajiunga Raja Casablanca

Kiungo wa kati Balla Conte amejiunga na timu ya Raja Casablanca ya Morocco ambayo ipo chini ya Kocha Fadlu Davids Balla Conte amejiunga na Raja Casablanca kwa mkopo wa miezi sita. Conte anaondoka leo Tanzania kuelekea Morocco Buba Jammeh amechukua nafasi ya Balla Conte. Yamga SC imefanikiwa kusalia na wachezaji 12 wa Kigeni kama kanuni inavyosema usajili wa Buba Jammeh dakika za mwisho kuchukua nafasi ya Balla Conte ambae Yanga ilimuachia kwa mkopo dakika za mwisho kabla ya dirisha dogo la Tanzania halijafungwa.

Gundu lamuandama Mayele, Pyramids

Zimepita siku 90 tangu mshambuliaji wa klabu ya Pyramids Fiston Kalala Mayele afunge goli akiwa na klabu hiyo mara ya mwisho kufunga goli ilikuwa mwezi Oktoba mwaka jana. Msimu uliopita Mayele alifunga magoli manne (4) kwenye michezo tisa (9) ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita na magoli nane (8) kwenye michezo 23 ya Ligi Kuu ya Misri

Mjue Nadir Haroub Ali Canavaro: Beki wa zamani Yanga na Taifa Stars, aliyejizolea sifa kemkem

NADIR Haroub Canavaro, ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa Tanzania nafasi yake Kiwanjani Ilikuwa ni Beki wa Kati (Center-defender) aliyezaliwa tarehe 10 Februari 1982, huko Michenzani, Zanzibar. Nadir Alikuwa mchezaji mwenye umaarufu mkubwa sana nchini Tanzania, aliichezea Young Africans SC kwa miaka mingi Takribani miaka 12, ambapo alivaa jezi namba 23 na kuwa nahodha (captain) wa timu hiyo na pia ya timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars). Mbali na Yanga Sc, Nadir alicheza Malindi ya Zanzibar, alikwenda Canada kwa mkopo (loan) kwa timu ya Vancouver Whitecaps, wakati huo ikijiandaa kujiunga na MLS). Hakupata mechi rasmi, na alirudi Tanzania baada ya muda mfupi kwa sababu hakufurahishwa na hali ya huko. Nadir alibaatizwa Jina lake la utani Canavaro, kutokana na mtindo wake wa kucheza kama beki hodari na mkali wa ulinzi, sawa na Fabio Cannavaro (mwitaliano aliyeshinda Ballon d'Or mwaka 2006). Nadir alicheza Timu ya Taifa (Taifa Stars) hadi alipoamua kustaafu kimataifa Machi...

Bubah Jammeh atambulishwa Yanga

KLABU ya Yanga imemtambulisha winga wa kulia anaweza kukikimbia na kushoto pia, Mgambia Bubah Jammeh (27) kutoka Interclube ya Angola kuwa mchezaji wake mpya katika dirisha hili dogo. Mchezaji huyo mwenye kipaji kikubwa pendekezo la Kocha Mreno wa timu hiyo, Pedro Valdemar Soares Gonçalves tayari yupo visiwani Zanzibar na timu hiyo ikijiandaa na mchezo wa leo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Afrika. Yanga inatarajiwa kushuka Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar kuanzia Saa 10:00 jioni ya leo kumenyana na Al Ahly ya Misri katika mchezo wa leo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Afrika. Bubah Jammeh anakuwa mchezaji mpya wa sitano Yanga dirisha hili dogo baada ya kiungo Mguinea Mohamed Damaro Camara kutoka Singida Black Stars aliyechukua uraia wa Tanzania, winga Mganda Allan Okello kutoka Vipers ya kwao na mshambuliaji, Muangola - Laurindo Dilson Maria Aurélio ‘Depú’ kutoka Radomiak Radom ya Poland. Wengine ni wazawa wawili, kipa Hussein Masalanga (33) kutoka Singida Black Stars (33) na mshambuliaji...

Simba yamalizana na straika la Ivory Coast

Simba amekamilisha usajili wa mshambuliaji raia wa Ivory Coast, Mofossé Trésor Karidioula, katika dirisha dogo la usajili kwa ajili ya msimu huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara Na Mashindano Ya kimataifa. Karidioula, mwenye umri wa miaka 27, amejiunga na kikosi cha simba huku akiwa na rekodi ya kucheza katika ligi mbalimbali za Afrika na uzoefu wa kimataifa. Mchezaji huyo aliitumikia klabu ya Haras El Hodood ya Misri msimu uliopita kabla ya kuwa huru, na sasa anaendelea na safari yake mpya akiwa Simba. Kabla ya kuichezea Misri, Karidioula alionyesha ubora wake akicheza kwa vilabu kama Williamsville AC na ASEC Mimosas ya Ivory Coast, Simba wamemsajili akitokea Marumo Gallants FC ya Afrika Kusini. Karidioula anacheza katika nafasi za mbele kama winger au mshambuliaji, akijulikana kwa kasi yake, mbinu bora ya kuvunja safu za ulinzi na uwezo wa kufunga na kusaidia mabao. Uzoefu wake mkubwa uwanjani unatarajiwa kuongeza nguvu kubwa katika safu ya ushambuliaji ya Simba, huku akiwa amevaa jezi namb...

Al Ahly wafanya mazoezi ya kuimaliza Yanga kesho

Al Ahly katika mazoezi yao ya mwisho leo kuelekea mchezo wao wa Marudiano dhidi ya Yanga hapo Kesho. Yanga itacheza kesho saa 10 jioni Katika uwanja wa New Aaman Complex Zanzibar.

JKT Tanzania yashindwa kuishusha Yanga kileleni

Timu ya JKT Tanzania imeshindwa kuishusha Yanga SC kileleni baada ya kufungwa bao 1-0 na Dodoma Jiji uwanja wa Meja Isamuyo Mbweni jijini Dar es Salaam mchezo wa Ligi Kuu bara. Bao pekee la Dodoma Jiji limefungwa na mshambuliaji wake hatari Wiliam Edgar dakika ya 50, kwa matokeo hayo JKT Tanzania inaendelea kubaki nafasi ya pili na pointi zao 21 wakati Yanga ikiongoza na alama 22. Wiliam Edgar

Yanga Princess yazidi kuipumulia Simba Queens kileleni

Yanga Princess imeendelea kuifukuzia Simba Queens katika msimamo wa Ligi Kuu ya wanawake Tanzania bara, baada ya leo kuifunga Bunda Queens mabao 3-1 uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. Magoli ya Yanga Princess yamefungwa na Jeannine Mukandayisenga aliyefunga mabao mawili na Aisha Djafar wakati bao la Bunda Queens limefungwa na Kulwa Rocket. Yanga Princess anamaliza raundi ya kwanza na ushindi mnono ugenini huku akiendelea kuwa nafasi ya pili chini ya Simba Queens. Bunda Queens wameganda pale pale wanaruhusu vipigo nyumbani mfululizo.

Clara Luvanga apiga hat trick nyingine Al Nassr

Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania Clara Luvanga hii leo ameifungia Hat Trick Klabu yake ya Al Nassr Women na kuisaidia kushinda 7-1 dhidi ya Eastern Flames kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake nchini Saudi Arabia . . Clara Luvanga amefikisha mabao 15 kwenye Ligi hiyo akiwa ndiye kinara wa mabao huku Klabu yake ikishika nafasi ya kwanza kwenye Msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 24 baada ya kucheza michezo minane.

Okwi aipongeza Yanga kumsajili Okello

Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Anorld Okwi, amefunguka na kuipongeza klabu ya Yanga kuinasa saini ya kiungo wa ushambuliaji, Allan Okello huku akidai kuwa wamefanya kazi kubwa na wamepata mchezaji bora. Kwani sio kitu rahisi kumshawishi rais wa klabu ya Vipers, Lawrence Mulindwa ambaye alikuwa akiamini watamuuza Okello barani Ulaya au nchi za Afrika ya Kaskazini kutokana na uwezo alionao. "Kwenye ukweli lazima useme kuwa va uongozi wa Yanga unastahili pongezi kwa usajii wa nyota Allan Okelo wa Uganda. Huku ni kukomaa kwa viongozi wa Yanga, kingine ni kitendo cha Rais wa Yanga, Eng. Hersi Saidi kuingilia kati mwenyewe kimemfanya Mulindwa kuwa mpole''. Alisema Okwi, ambaye pia amewahi kukipiga Yanga SC.

Mshambuliaji Yanga Princess avunja rekodi yake mwenyewe aliyoiweka

Jeannine Mukandayisenga amevunja rekodi yake yeye mwenyewe aliyoiweka msimu pita akifunga mabao 13 kumbuka alicheza mzunguko mmoja tu aliingia Yanga dirisha kubwa la usajili. Jeannine Mukandayisenga alifunga mabao 13 ya ligi wakati pia akifunga mabao matatu (3) kwenye michuano ya Samia Cup akimzidi Neema Poul aliyefunga magoli 12 kwa sasa yupo Fountain baada ya kuondoka Yanga. Msimu huu ligi pekee amefunga mabao 16 katika michezo 11 ya nusu msimu Ni wachezaji wawili tu wakigeni hadi sasa ambao wamefanikiwa kutwaa tuzo ya mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania kwa misimu miwili tofauti mfululizo. Jentrix Shikangwa (kutoka Kenya) na Asha Djafari (kutoka Burundi) wote walitwaa wakiwa Simba Queens. 2019/2020 – Fatuma Mustapha (JKT Queens): mabao 33 Mzawa. 2020/2021 – Aisha Masaka (Yanga Princess): mabao 35 Mzawa. 2021/2022 – Asha Djafari (Simba Queens): mabao 26 2022/2023 – Jentrix Shikangwa (Simba Queens): mabao 17 2023/2024 – Aisha Mnunka (Simba Queens): mabao 20 Mzawa. 2024-2025...

Hatutegemei mtelemko kuwafunga Al Ahly kisa kumkosa Ashour- Pedro

Kocha mkuu wa Yanga SC Pedro Goncalves amesema kukosekana kwa mchezaji Emam Ashour katika cha Al Ahly akimpi matumaini ya kushinda dhidi yao, isipokuwa wanajipanga Ili wafanye vizuri siku ya mchezo, kesho. "Ili ufanikiwe katika Ligi ya Mabingwa Afrika na ukicheza dhidi ya timu kama Al Alhy ni lazima uwe tayari kwa kila aina ya nyakati ndani ya uwanja. Kutokuwepo kwa Ashour hilo ni tatizo lao Al Ahly sisi jukumu letu ni kujiandaa vyema.” - "Kabla ya yote tulipopangwa kwenye kundi hili kila timu ilifahamu ipo kwenye kundi gumu, sisi kama Young Africans kazi yetu ni kupambana na kila timu ili kujiweka kwenye sehemu nzuri tunapaswa kuwa bora, makini na tayari kucheza mpira mzuri ili kuwa sehemu nzuri, kuhusu mechi ya kwanza ni kweli tulicheza vizuri lakini tulifanya makosa machache ambayo kwa ubora wa wapinzani wetu walituadhibu. Hapo kesho tunapaswa kuonesha ukuaji na ubora wetu pia ili kushinda

Kilichomkuta Emam Ashour Al Ahly hiki hapa

Emam Ashour Ana ugomvi mkubwa na kocha mkuu wa Al Ahly,hii ilitokea kati kati ya juma kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya Wadi Degla,baada ya mchezaji huyo kumtukana kocha wakati alipofanyiwa mabadiliko dakika 69 ya mchezo. Kocha Jess Thorup alikasirishwa na tabia ya nyota huyo na kumchana kwamba hatokuwa sehemu ya kikosi kitakacho kuja Tanzania kuivaa Yanga. Baada ya hapo kulitokea msuguano mkubwa kati ya kocha Jess Thorup na uongozi wa Al Ahly Baada uongozi kuonyesha wazi unamkingia kifua na kumtaka mchezaji huyo ajumuishwe kwenye Safari ya kuja Tanzania. Jana uongozi ulijumuisha jina la Emam Ashour kwenye list ya Wachezaji watakao kuja Tanzania Ila mpaka safari inaanza Emam Ashour,hajaonekana hivyo kijana amekataa amri ya viongozi na kubaki nyumbani,ndio maana amelimwa adhabu. Pamoja na uwezo wake uwanjani Ila Emam Ashour ni mtukutu mno

Azam FC yaichapa TRA United

Timu ya Azam FC usiku huu imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya TRA United ya mkoani Tabora mchezo wa Ligi Kuu bara uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam. Mabao ya Azam FC yamefungwa na Jean Ngita raia wa DR Congo dakika ya 39 na Iddi Nado dakika ya 90, kwa matokeo hayo Azam FC imefikisha pointi 16 ikicheza mechi 8.

Wachezaji wengi wa Afrika magharibi wanahamia Afrika Kusini kwa sababu ya pesa- Nwabali

Golikipa wa Nigeria na klabu ya Chippa United ya South Afrika Stanley Nwabali amesema wachezaji wengi wa Afrika Magharibi huhamia Ligi ya Afrika Kusini kwa sababu inalipa vizuri na iko kwenye kiwango cha juu. Kwa mujibu wake anasema Ligi ya Afrika Kusini na Morocco ni bora kuliko ligi nyingi za Afrika Magharibi. Ndiyo maana wachezaji wa ligi hizo hawana presha ya kukimbilia Ulaya, kwa sababu tayari wanapata mazingira mazuri na malipo bora.

Diva The Boss wa Wasafi Media ajiunga EFM

Aliyekuwa mtangazaji wa redio na televisheni ya Wasafi Media, Diva The Boss amejiunga na redio ya EFM. Hivi karibuni kumekuwa na hama hama ya watangazaji maarufu wa Wasafi Media, Diva The Boss naye alikuwa miongoni mwao lakini tayari EFM wameshaingia naye kandarasi.

Al Ahly yaipa unafuu Yanga

Al Ahly imemsimamisha kiungo wao Emam Ashour kwa muda wa wiki mbili na imemtoza faini ya EGP 1.5 m (TshsMilioni82) kwa kushindwa kusafiri na timu leo kuja Tanzania kwaajili ya kuwakabili Yanga. Emam atafanya mazoezi peke yake katika kipindi chote cha kifungo.

Wachezaji wa zamani nchini walifurika kwa wingi kumzika Peter Manyika

Nyota mbalimbali wa mchezo wa soka hapa nchini waliotamba zamani na wa sasa, jana walifurika kwa wingi kumsindikiza gwiji mwenzao wa soka mlinda mlango nambari moja miaka ya 90 Peter Manyika aliyezikwa jana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam. Picha zote ni kwa hisani ya Lubigisa Lubigisa beki wa zamani wa Simba SC.