Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mshambuliaji Yanga Princess avunja rekodi yake mwenyewe aliyoiweka

Jeannine Mukandayisenga amevunja rekodi yake yeye mwenyewe aliyoiweka msimu pita akifunga mabao 13 kumbuka alicheza mzunguko mmoja tu aliingia Yanga dirisha kubwa la usajili.

Jeannine Mukandayisenga alifunga mabao 13 ya ligi wakati pia akifunga mabao matatu (3) kwenye michuano ya Samia Cup akimzidi Neema Poul aliyefunga magoli 12 kwa sasa yupo Fountain baada ya kuondoka Yanga.

Msimu huu ligi pekee amefunga mabao 16 katika michezo 11 ya nusu msimu

Ni wachezaji wawili tu wakigeni hadi sasa ambao wamefanikiwa kutwaa tuzo ya mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania kwa misimu miwili tofauti mfululizo.

Jentrix Shikangwa (kutoka Kenya) na Asha Djafari (kutoka Burundi) wote walitwaa wakiwa Simba Queens.

2019/2020 – Fatuma Mustapha (JKT Queens): mabao 33 Mzawa.

2020/2021 – Aisha Masaka (Yanga Princess): mabao 35 Mzawa.

2021/2022 – Asha Djafari (Simba Queens): mabao 26

2022/2023 – Jentrix Shikangwa (Simba Queens): mabao 17

2023/2024 – Aisha Mnunka (Simba Queens): mabao 20 Mzawa.

2024-2025 -- Stumai Abdallah (Jkt Queens) : Mabao 27 Mzawa.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa