Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ARSENAL WAWEKWA KUNDI MOJA NA BAYERN

Olivier Giroud 

Arsenal watakutana na Bayern Munich Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya tatu katika misimu minne baada ya kuwekwa pamoja na klabu hiyo ya Ujerumani hatua ya makundi.

Manchester United watakabiliana na PSV Eindhoven wanaporejea tena dimba hilo kuu la Ulaya, mshambuliaji wao mpya Memphis Depay akilazimika kukabili klabu aliyotoka kabla ya kuhamia Old Trafford.

Chelsea nao watakabiliana na Porto, ambao kocha wao Jose Mourinho aliongoza kushinda dimba hilo 2004.

Manchester City wamepangwa kundi moja na Juventus kutoka Serie A, mabingwa wa Europa League Sevilla na Borussia Monchengladbach ya Ujerumani. Vijana wa Arsene Wenger pia watakutana na Olympiakos ya Ugiriki na Dinamo Zagreb ya Croatia.


Kando na PSV, United watakutana pia na klabu ya CSKA Moscow kutoka Urusi na klabu iliyomaliza ya pili ligi ya Ujerumani Wolfsburg.

Kundi la Mourinho Chelsea linakamilishwa na mabingwa wa Ukraine Dinamo Kiev na Maccabi Tel Aviv ya Israel.

Droo kamili: 

Kundi A: Paris Saint-Germain, Real Madrid, Shakhtar Donetsk, Malmo
Kundi B: PSV, Manchester United, CSKA Moscow, Wolfsburg
Kundi C: Benfica, Atletico Madrid, Galatasaray, Astana
Kundi D: Juventus, Manchester City, Sevilla, Borussia Monchengladbach
Kundi E: Barcelona, Bayer Leverkusen, Roma, BATE Borisov
Kundi F: Bayern Munich, Arsenal, Olympiacos, Dinamo Zagreb
Kundi G: Chelsea, Porto, Dynamo Kiev, Maccabi Tel-Aviv
Kundi H: Zenit St Petersurg, Valencia, Lyon, Gent.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa