Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2026

Kipre Jr awafuata Aziz Ki, Mukwala na Ngoma, Libya

Aliyekuwa winga wa klabu ya Azam FC na MC Alger raia wa Ivory Coast Kipre Zuon Junior amejiunga na klabu ya Al Nasry ya Ligi Kuu ya Libya, Kipre Jr amejiunga na klabu ya Al Nasry baada ya kuachana na waliokuwa waajiri wake MC Alger kwa makubaliano ya pande zote mbili, Sasa rasmi amejiunga na klabu ya Al Nasry kwa mkataba wa msimu mmoja na nusu, Kipre Jr anaungana na Fabrice Ngoma, Nathan Fasika, Steve Mukwala na Khadim Diam ambao wote wamesajiliwa Al Nasry

Yanga inahitaji kuifunga FAR Rabat wafuzu moja kwa moja robo fainali

Mechi ijayo ni fainali kwa Yanga, kwanza wanahitaji ushindi ili wafuzu moja kwa moja bila kusubiri matokeo ya mechi ya mwisho, (endapo JS Kabylie atashindwa kumfunga Al Ahly) ,pili Yanga,wakishindwa kumfunga FAR Rabat . Basi Yanga wapambanie sare kisha wasubiri kushinda mechi yao mwisho ili wafuzu ,au wamuombee mabaya FAR Rabat kwenye mechi yake ya mwisho dhidi ya Ahly, na tatu Yanga wakifungwa basi wasifungwe kwa tofauti ya goli moja maana wakifungwa 2-0, 3-1 na kuendelea mchezo utakuwa umeisha na FAR Rabat watasonga mbele kwa H2H bila hata kusubiri matokeo ya mwisho. Mechi ijayo ni fainali kwa Yanga,faida kwao ni kwamba FAR Rabat hawatokuwa na mashabiki…..hivyo Yanga wakaze.

Alphonce Mabula azidi kukiwasha huko Azerbaijan

Nyota wa Tanzania Alphonce Mabula na timu yake ya FC Shamakhi wamepata alama tatu kwenye ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kapaz kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Azerbaijan