Rais Wallace Karia atembelea mradi wa Barrick Tanzania, Buzwagi
Rais wa TFF Wallace Karia akiongozana na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji TFF na Katibu Tawala Wilaya ya Kahama Glory Absalum leo wametembelea Mradi wa ufungwaji wa Barrick Tanzania, Buzwagi uliopo Kahama, Shinyanga kutazama miundombinu iliyopo kwa ajili ya kuanzisha Kituo cha Soka kuendeleza vipaji vya mpira wa miguu






