KIUNGO wa Kimataifa wa Uganda, Khalid Aucho amesema kwenye maisha yake ya soka hajawahi kuhusishwa na utovu wa nidhamu kwa namna yoyote.
Aucho ameandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kufuatia taarifa ya klabu ya klabu yake, Singida Bkack Stars kumsimamisha yeye na kipa Mnigeria, Amas Daniel Obasogie kwa tuhuma za utovu wa nidhamu.
“Nimekuwa nikizingatia taaluma yangu kila wakati katika taaluma yangu, nikiiwakilisha kila klabu kwa heshima na nidhamu.
Katika miaka yangu yote katika soka, sijawahi kuhusika katika kesi yoyote ya utovu wa nidhamu kwa sababu ninaelewa jukumu linalokuja na kuwa mchezaji mwadilifu.
Kwa mashabiki wangu wapendwa ambao wamekuwa wakiniunga mkono kila wakati, hali litapita. Asante kwa msaada wako unaoendelea,” amesema mchezaji huyo wa zamani wa Yanga.
