Hasheem Thabit achaguliwa kuwa Rais wa TBF


Nyota wa basketball Tanzania, Hasheem Thabeet amechaguliwa kuwa rais wa chama cha mpira wa kikapu Tanzania (TBF) baada ya kushinda kinyanganyiro hicho katika uchaguzi uliofanyika leo jijini Dodoma.

Katika uchaguzi huo Hasheem ameibuka mshindi baada ya kupata kura 34 kati ya 60 zilizopigwa na wajumbe wote.

Hashem kwa sasa anachezea timu ya kikapu ya Dar City ambayo inatarajiwa kucheza fainali za ‘BAL’ kwenye michezo itakayochezwa kuanzia Machi 27 nchini Afrika Kusini.

Wengine walioshinda katika uchaguzi huo Mohamed Kisui (Makamu wa Rais), Mwenze Fiston Kabinda (Katibu Mkuu) na Simon Milondo (Naibu Katibu Mkuu).

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI