-Kwamba Simba walikubaliana na Wydad Ac Usd 120,000 sawa na Milioni 316 kwajili ya mkataba wa mkopo wa mwaka mmoja wa mchezaji Selemani Mwalimu. Simba walikuwa tayari kutoa hiyo pesa ndio maana mchezaji akaruhusiwa kurudi Tanzania na akafikia kwenye Kambi ya Simba ambako alikuwepo mpaka jana kwenye mazoezi ya Simba pale Zanzibar. Yanga walivyopata taarifa za Simba kuchelewa kufanya malipo, wakaulizia wakaweka mezani Usd 200,000 (Milioni 527) yaani Usd 80,000 zaidi ya ile pesa waliyokubaliana na Simba...Wydad wakampigia simu Mwalimu kumwambia awaambie Simba kuna timu imeweka 200,000 hivyo Simba waongeze Usd 30,000 tu iwe Usd 150,000 (Milioni 395) Selemani Mwalimu alivyowaambia viongozi wa Simba, wakamwambia wanawachekecha tu kwasababu Yanga hawana uhitaji wa mshambuliaji tena... Baadaye Viongozi wakampigia simu Mwalimu kumwambia wamemalizana na Yanga hivyo anatakiwa kurudi Dar, ndipo akaondoka na ndege ya usiku kurudi Dar na alisaini mkataba na Yanga saa 9:45 usiku. Usd 30,000 ndiyo il...