Depu atambulishwa Petro de Luanda
Mshambuliaji raia wa Angola, Laurindo Aurélio maarufu Depu, ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa Petro de Luanda baada ya kuondoka Yanga.
Depu ametambulishwa rasmi leo Jumatano Agosti 12, 2026 ambapo inadaiwa Yanga imeingiza kitita cha dola 500,000 (Sh1.3 bilioni) kwa ajili ya usajili wa mchezaji huyo.
Depu alikuwa sehemu ya kikosi cha Yanga msimu uliopita kabla ya kurejea nchini Angola kujiunga na Petro de Luanda.
