Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIMONDO YAZIDI KUIWEKA ROHO JUU YANGA

Wakati uongozi wa Yanga umedai kuwa ulimsajili kiungo Geofrey Mwashiuya akiwa huru, uongozi wa Kimondo umesema una mkataba na mchezaji huyo na utawashtaki mabingwa hao wa Bara ikiwa wataendelea kumtumia.

Mwanzoni mwa wiki Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, Jerry Muro aliwaambia waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18, alisaini nayo mkataba wa miaka mitatu akiwa huru.

Hata hivyo, mkurugenzi wa Kimondo, Elick Ambakisye aliuambia mkutano na waandishi wa habari jijini hapa jana kuwa Mwashiuya ana mkataba wa miaka minne aliousaini Agosti 30 mwaka jana.


"Mchezaji (Mwashiuya) mwenyewe alisaini mkataba huu (anauonyesha). Endapo Yanga wataendelea kumng'ang'ania na kumtumia mchezaji wetu, tunajua wanashiriki Kombe la Kagame mwezi huu, tutawashtaki katika mamlaka husika," alisema Ambakisye.

Kombe la Kagame la klabu bingwa ya Afrika Mashariki na Kati linashirikisha wachezaji waliosajili na kupata leseni za kuzitumikia klabu.

Hivyo ni wazi kwamba Yanga haitamtumia Mwashiuya kwa sababu usajili wake bado haujaidhinishwa na Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka (TFF).

Mwashiuya alijiunga na Yanga mwezi uliopita na kuibua mvutano kati ya viongozi wa timu yake hiyo mpya na Kimondo.

Kiungo huyo anayetumia mguu wa kushoto alionyesha kiwango kizuri katika mechi yake ya kwanza ya kiamataifa ya kirafiki ambayo Yanga ilitoka suluhu na SC Villa ya Uganda, kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi iliyopita.

Mbali na Mwashiuya, Yanga imesajiliwa pia wachezaji wazawa wengine Deus Kaseke kutoka Mbeya City, Malimi Busungu (Mgambo JKT), Benedicto Tinocco (Kagera Sugar) na Haji Mwinyi Mgwali (KMKM).

Pia imewachukua Mzimbawe Donald Ngoma na Mghana Josephat 'Teteh' Zhuta.

Mbali na Kombe la Kagame ambako Yanga itakuwa ikiwania kufikia rekodi ya watani wa jadi ya kuchukua ubingwa mara ya sita, timu hiyo inajiandaa kutetea taji la ligi kuu ya Bara na kucheza Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwakani.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe