Machapisho

Masikini Kibabage!!

Picha
Simba SC imepata pigo baada ya beki wake, Nickson Kibabage, kupata majeraha yatakayomuweka nje ya uwanja kwa takribani wiki 3–4. Tunamtakia Kibabage ahueni ya haraka na tunatarajia kumuona ak irejea uwanjani akiwa fiti zaidi.

Mayele aibukia Al Ahli Tripoli

Picha
Mshambuliaji wa kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Fiston Kalala Mayele, amejiunga rasmi na klabu ya Al Ahli Tripoli ya Libya akitokea Pyramids FC ya Misri kama mchezaji huru. Mayele amesaini mkataba wa miaka miwili, utakaomuweka klabuni hapo hadi Juni 2028. Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na vyanzo mbalimbali vya michezo, thamani ya jumla ya kifurushi cha mkataba wake inakadiriwa kufikia Dola Milioni 5 kwa miaka miwili. Mshahara wa milioni 550 kwa mwezi pale Al Ahly Tripoli SC ambao ukiugawanya unapata around 19.7 m kwa siku  Fiston Kalala Mayele amegonga jackpot baada ya kipaji na juhudi zake,19.7m kwa siku pungufu ya 1.3m mshahara wa mwezi aliokuwa akipokea Young Africans SC (21m monthly)

Injinia Hersi amkabidhi gari mbunifu idara ya habari

Picha
Rais wa Yanga, Eng. Hersi Said, amemkabidhi zawadi ya gari Willy Shemoka @shemokawilly kama pongezi kwa kutokana na jitihada zake na ubunifu mkubwa alionesha kwenye idara ya habari. Mafanikio haya yanaenda sambamba na ubunifu, bidii na maboresho makubwa katika uzalishaji wa maudhui ya Yanga. Kama muandaa maudhui , Willy amekuwa sehemu muhimu ya safari hii, huku YouTube ya Yanga ikifikia hadhi ya kuwa namba moja Afrika kwa watazamaji. Hongera Willy Shemoka

Shalulile azua balaa Mamelodi

Picha
Mashabiki wa Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini wameanza kutoa milio na wakionekana kuushutumu uongozi wa timu kumuachia aondoke. Mashabiki hao wa Mamelod ya wameanza kuulamu uongozi wao pamoja na kocha wa timu yao Miguel Cardozo kwa kumuacha Peter Shalulile kutimkia Young Africans Sports Club ya Tanzania na kubaki na Mothiba ambae kiwango chake hawajaridhishwa nacho.

Coastal wagumu lakini tutashinda- Matola

Picha
Kocha Msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola, amesema mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Coastal Union utakuwa mgumu, lakini kikosi chake kimejiandaa kuhakikisha kinapata alama tatu. Matola amesema licha ya Coastal Union kutokuwa na matokeo mazuri katika michezo yake ya mwanzo, timu hiyo imekuwa ikionesha ushindani mkubwa inapokutana na Simba SC. Akizungumzia matumizi ya Video Support (FVS), Matola amesema teknolojia hiyo imeongeza kitu katika ligi, huku benchi la ufundi likiwataka wachezaji kuongeza umakini na kuepuka makosa yanayoweza kuonekana kupitia mfumo huo. Kwa upande wake, golikipa wa Simba SC, Hussein Abel, amewahakikishia Wanasimba kuwa wataingia uwanjani kupambana kupata alama tatu na kulinda lango lao bila kufungwa. Simba SC itakutana na Coastal Union kesho, Agosti 27, 2026, saa 1:00 usiku katika Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam. Taarifa rasmi ya Simba SC pia inaonesha kuwa mchezo huo utaanza saa 1:00 usiku.

Kiungo wa Morocco atua Manchester City

Picha
Kiungo wa kimataifa wa Morocco, Ayyoub Bouaddi, mwenye umri wa miaka 18, amekamilisha uhamisho wake kutoka Lille ya Ufaransa kwenda Manchester City, katika dili lenye thamani ya jumla ya euro milioni 100. Manchester City imelipa euro milioni 95 kama ada ya awali, ambapo ni sawa na Shilingi bilioni 293.15 za Tanzania huku euro milioni tano zikitarajiwa kulipwa kupitia bonasi zinazoweza kufikiwa kulingana na utendaji wa mchezaji na klabu. Bouaddi amesaini mkataba wa miaka mitano utakaomuweka Etihad Stadium hadi mwaka 2031. Uhamisho huo umemfanya Bouaddi kuwa kijana mwenye umri mdogo zaidi aliyewahi kusajiliwa kwa gharama kubwa zaidi katika historia ya Premier League, akivunja rekodi iliyowekwa na Leny Yoro, ambaye alihama Lille kwenda Manchester United kwa euro milioni 70 mwaka 2024. Bouaddi anakuwa mchezaji wa pili mkubwa kusajiliwa na Manchester City katika eneo la kiungo katika dirisha hili la usajili, baada ya Elliot Anderson kujiunga na klabu hiyo akitokea Nottingham Forest. Akizung...

Kenya yataka mechi za ufunguzi

Picha
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Nicholas Musonye, amesema Kenya ina uwezo wa kuandaa mechi ya ufunguzi na fainali ya AFCON 2027. Hii ni wakati ambapo maandalizi ya pamoja ya Kenya, Uganda na Tanzania (PAMOJA) kwa AFCON 2027 yanaendelea kushika kasi.