Machapisho

MAKALA: Mashabiki wa soka nchini wajifunze kushangilia

Picha
Na Prince Hoza SIKU kumekuwa na tabia mbaya hasa kutoka kwa mashabiki wa soka hapa nchini kujifanya wakosoaji badala ya kusimama kwenye maeneo yao ya ushangiliaji.  Mashabiki wa soka hasa wa hapa nchini, wamekuwa wakisifika kwa kupenda sana mchezo huo na kuisaidia nchi kuonekana ina mashabiki wengi wanaoufuatilia zaidi mchezo huo.  Lakini bahati mbaya, mashabiki wa soka wa hapa nchini wanaishia kujitokeza kwa wingi viwanjani na hata kwenye vibanda umiza, yote kuzisapoti timu zetu lakini hawajui kushangilia kama inavyotakiwa na zaidi wamejikita  kwenye kukosoa.  Yaani mashabiki wa soka nchini wamegeuka wachambuzi na badala yake wamekuwa wakikosoa timu zao, wapo mashabiki wamejifanya wakosoaji wa timu ya taifa, Taifa Stars, hasa wakimkosoa kocha mkuu wa timu hiyo katika uteuzi wake alioufanya hivi karibuni.  Pia wapo wengine wakimkosoa kocha wa timu ya Simba SC, Robert Olveira "Robertinho", na wengine wanamkosoa kocha wa timu ya Yanga SC Nasreddine Nabi, kwa kifupi mashabiki wa...

CHELSEA YAFUTURISHA WAISLAMU UINGEREZA

Picha
Klabu ya Chelsea imekuwa Klabu ya kwanza nchini Uingereza kuruhusiwa na kutumika kwa ajili ya kula Iftar kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Lakini pia Uwanja wa Chelsea wa Stamford Bridge umekuwa ni uwanja wa kwanza wa timu ya ligi kuu ya England kutumika kwa ajili ya Kuftar kwenye mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Mzize apigiwa chapuo Taifa Stars

Picha
Na Salum Fikiri Jr Aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Sheria na Utawala wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Eliud Mvella amesema kama taifa tunapaswa kuanza kuaanda mshambuliaji wa kati atakaye mrithi mshambuliaji Johh Rafael Bocco, na amesisitiza kuwa mshambuliaji kinda wa Yanga Clement Mzize ndiyo mbadala sahihi wa Bocco. ‘’Hatuna mchezaji wa kusimama mbele kwa sababu Mbwana Samatta anatakiwa acheze nyuma ya mtu (Inside ten) lakini lazima tuwe na mtu mwenye uwezo, nguvu na uwezo wa kumiliki mpira kama ilivyokuwa Bocco. Ni muhimu sana lakini ugonjwa huu utatibika siku si nyingi kama walimu wakikaa na wakamtengeneza yule kijana Clement Mzize wa Yanga. Mimi naamini Yule ndo atakuwa tiba. Lazima TFF wa mwambie mwalimu wa timu ya Taifa’’ Amesema Mvella.

Mo Dewji anunua tiketi 5000, kesho atakufa mtu

Picha
"Rais wa heshima wa Simba, Mohamed Dewji amenunua tiketi 5000,Wadhamini wa Simba SC AfriCarriers wamenunua tiketi 2000 wakati Azim Dewji na wafanyakazi wa kampuni yake wamenunua tiketi 1000 lengo ni kuhakikisha mashabiki wanaujaza Uwanja wa Mkapa kesho na kuhamasisha tunamfunga Uganda" Clifford Ndimbo , Afisa Habari wa TFF

Stars kamili kuiua Uganda kesho

Picha
Na Ikram Khamees Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania leo hii kimeendelea na mazoezi tayari kwa kujiandaa kuelekea mchezo wa marudiano wa kufuzu AFCON dhidi ya timu ya Taifa ya Uganda, mchezo huo utachezwa siku ya Jumanne ya tarehe 28/03/2023 katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Tanzania. Kwahiyo kocha Adel alikuwepo miezi miwili kabla ya kutangazwa kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania kama anavyosema Rais wa shirikisho la mpira wetu TFF Wallace Karia? na alikuwa anawatazama baadhi ya wachezaji wakati ligi zinaendelea, sasa ndani ya hiyo miezi miwili hakuona umuhimu na ubora wa walinzi wawili wa pembeni Shomari Kapombe na Mohamed Hussein?. Badala yake akaona ubora wa kina Datus Peter, Kibwana Shomari kama mabeki wa kulia, na kushoto akawaona David Charles Luhende na Yahya Suleiman Mbegu? kwahiyo kocha aliangalia zaidi mechi za Kagera Sugar na Ihefu kuliko mechi za Simba? maana kwa maelezo ya Rais wetu wa heshima kasema hata kikosi ni mwalimu alikiita. Na ukiangalia wache...

Niyonzima anaendelea kutesa Uarabuni

Picha
Kiungo fundi wa zamani wa Simba na Yanga,Haruna Niyonzima hapo juzi aliibuka Mchezaji Bora wa Mechi baada ya kuonesha Kiwango Bora zaidi na akitoa Assist Moja wakati timu yake ya Al Taawon SC ikilazimishwa sare ya goli 2-2 dhidi ya Al Akdhar kwenye Ligi Kuu Nchini Libya. Niyonzima alicheza kwa dakika 80 kwenye Mchezo huo na wakati anafanyiwa mabadiliko timu yake ilikuwa inaongoza kwa goli 2-0.

Hii ndiyo ndege binafsi ya Messi

Picha
Hii ndio ndege binafsi anayotumia Nyota wa Argentina Lionel Messi inayokadiriwa kuwa na thamani ya dola za Kimarekani milioni 15. Ndege hiyo ya kifahari ina majina ya familia kwenye ngazi yani Leo, mkewe Antonela na watoto wao Thiago, Ciro na Mateo. Vilevile ina nambari 10 mkiani, namba ambayo imekuwa alama kwa nyota huyo ikiwa ni namba aliyoitumia kwa muda mrefu wakati akiichezea FC Barcelona. Ndani yake kuna jiko, mabafu mawili na viti vya kutosha watu 16.Viti hivyo vinaweza kukunjwa na kugeuka kuwa vitanda 8. Ndege hii haimilikiwi na Messi bali ameikodisha na anaitumia yeye tu, hivyo haikodishwi kwa mtu mwingine yoyote kwa sasa. Usafiri huu wa haraka unamsaidia sana nyota huyo ukizingatia ratiba zake ngumu ambapo anatakiwa kuwepo sehemu tofauti duniani mara kwa mara kuhudhuria hafla mbalimbali, kucheza soka na kufanya kazi za chapa kadhaa anazoziwakilisha. Isitoshe inamuwezesha kusafiri na familia yake pamoja na marafiki kwenye mapumziko