Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Pazia la Ligi Kuu Bara kufungwa leo

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Pazia la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/18 linafungwa leo kwa mechi nane kupigwa katika viwanja mbalimbali hapa nchini, ligi hiyo inafikia tamati ikiwa bingwa ameshapatikana ambaye ni Simba SC.

Vita pekee iliyosalia ni ya kumsaka mshindi wa pili ambayo inawaniwa vikali na timu za Azam Fc na Yanga Sc ambao leo wanaumana usiku katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambapo Azam wana pointi 55 na Yanga ina pointi 52 hivyo nafasi iko wazi kwa Yanga endapo itashinda ila Azam inahitaji sare.

Pia vita ipo kwa timu mbili za Ndanda Fc ya Mtwara na Majimaji Songea ambapo moja leo itaungana na Njombe Mji kushuka daraja.

Ratiba kamili hii hapa

Yanga Sc vs Azam Fc Uwanja wa Taifa Dar es Salaam kuanzia saa 2;00 usiku.

Majimaji Fc vs Simba SC uwanja wa Majimaji Stadium mjini Songea.

Kagera Sugar vs Lipuli Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Tanzania Prisons vs Singida United Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

Ndanda Fc vs Stand United Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mtibwa Sugar vs Mbeya City Uwanja wa Manungu Complex mjini Morogoro.

Mbao Fc vs Ruvu Shooting Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Njombe Mji vs Mwadui Fc Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe na hii itakuwa mechi ya mwisho ya Ligi Kuu kuchezwa mjini Njombe

Ligi Kuu Bara inamalizika leo kwa timu zote 16 kushuka uwanjani

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa