Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba yamaliza kwa sare, Majimaji na Njombe zaipa kisogo Ligi Kuu Bara

Na Prince Hoza. Dar es Salaam

Timu ya soka ya Simba Sc ya jijini Dar es Salaam jioni ya leo imemaliza Ligi Kuu Bara kwa heshima ya aina yake baada ya kuilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 Majimaji Fc katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Kwa matokeo hayo Simba imefikisha pointi 69 na ikiwa mabingwa wa Tanzania Bara msimu huu huku timu ya Majimaji ikiwa imetelemka daraja ikiungana na Njombe Mji, Majimaji walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia Marcel Kaheza kabla ya Simba kusawazisha kwa penalti kupitia Haruna Niyonzima ambaye pia alikosa penalti iliyotaka kuzaa bao la pili iliyppanguliwa na kipa wa Majimaji, Hashim Mussa.

Matokeo mengine Mbao Fc 1 Ruvu Shooting 1 uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mtibwa Sugar 0 Mbeya City 0 Uwanja wa Manungu Complex mjini Morogoro.

Kagera Sugar 2 Lipuli 0 uwanja wa Kaitaba mjini Kagera.

Ndanda Fc 3 Stand United 0, Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mwadui Fc 2 Njombe Mji 0 Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.

Tanzania Prisons 1 Lipuli 0 Uwanja wa Sokoind mjini Mbeya.

Mpambano mwingine wa kufunga pazia la ligi utafungwa usiku wa leo kati ya Yanga Sc na Azam Fc uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam

Simba imemaliza ligi kwa heshima baada ya kutoka sare na Majimaji 1-1 leo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa