Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Majina ya wachezaji 30 watakaowania tuzo za VPL hawa hapa

Na Asher Maliyaga. Dar es Salaam

Shirikisho la mpira wa miguu nchini, TFF limetangaza jumla ya wachezaji 30 wanaocheza Ligi Kuu Bara hapa nchini watawania tuzo mbalimbali za wachezaji bora kwa mwaka huu inayotarajiwa kutolewa Juni 23 mwaka huu katika ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Afisa Habari wa Shirikisho hilo, Clifford Ndimbo imesema kwamba kufanyika kwa tuzo ni utaratibu ambao Shirikisho la mpira wa miguu hapa nchini, TFF limejiwekea kila mwaka baada ya kumalizika Ligi Kuu.

Tuzo hizo zitatolewa chini ya wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi, Vodacom na Azam Tv huku wakiongezeka wadhamini wengine ambao ni benki ya KCB na Primier Bet, alisema Ndimbo. Aidha Ndimbo amedai TFF imefuta tuzo ya mchezaji bora wa kigeni.

Licha ya kufutwa tuzo hiyo, Ndimbo amesema kutakuwa na tuzo mbalimbali za wachezaji bora, tuzo zirakazotolewa ni Timu yenye nidhamu, Mchezaji bora chini ya umri wa miaka 20, (Ismail Khalfan), Mchezaji bora chipukizi, Mwamuzi bora, Kipa bora, Kocha bora, Bao bora, Kikosi bora cha wachezaji 11 wa Ligi Kuu na mchezaji wa heshima.

Kamati ya tuzo imetaja majina ya wachezaji hao 30 watakaoshindanishwa kwenye tuzo hizo ambao ni Habibu Kiyombo (Mbao Fc), Khamis Mcha (Ruvu Shooting), Yahya Zayed, Razack Abalora, Bruce Kangwa, Himid Mao wote wa Azam Fc, Awesu Awesu (Mwadui Fc), Adam Salamba (Lipuli) Mohamed Rashid (Prisons), Shafik Batambuze, Mudathir Yahya, Tafadzwa Kutinyu wote wa Singida United.

Wengine ni Marcel Kaheza (Majimaji), Ditram Nchimbi (Njombe Mji), Eliud Ambokile (Mbeya City), Shaaban Nditi, Hassan Dilunga wa Mtibwa Sugar, Ibrahim Ajib, Gardiel Michael, Obrey Chirwa, Papy Tshishimbi na Kelvin Yondan wa Yanga SC, Aishi Manula, Emmanuel Okwi, John Bocco, Jonas Mkude, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya na Asante Kwasi wote wa Simba ambayo jumla imetoa wachezaji saba ikifuatiwa na Yanga na Azam kila moja ikitoa watano

Tuzo za wachezaji bora VPL zitatolewa Juni 23 mwaka huu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa