Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ngasa kuinusuru Ndanda kushuka daraja leo!

Na Mrisho Hassan. Dar es Salaam

Winga wa zamani wa kimataifa wa Tanzania aliyepata pia kung' ara katika vilabu vya Toto Africans ya Mwanza, Kagera Sugar ya Bukoba, Yanga, Azam na Simba za Dar es Salaam pamoja na Free State ya Aftika Kusini, Fanja ya Oman na Mbeya City ya Mbeya, Mrisho Khalfan Ngasa leo atakuwa na majukumu mazito ya kuinusuru timu yake ya sasa ya Ndanda FC ya mjini Mtwara itakaposhuka uwanjani kuwaalika Mwadui FC ya Shinyanga mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Mchezo huo unataraji kuanza saa 10:00 jioni kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara macho yote yataelekezwa kwa mkali huyo aliyewahi pia kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika klabu ya West Ham ya Uingereza huku pia akiwa na rekodi ya kucheza na Manchester United alipojiunga kwa muda na timu ya Seatle Sounders ya Marekani.

Mbali ya Ngasa, Ndanda pia inamtegemea mshambuliaji wake Omari Mponda ambaye atawasuuza wakazi wa Mtwara, hivi karibuni Mwadui iliifunga Yanga bao 1-0 hivyo leo itakuwa kazi nyepesi kwa Ndanda, Ndanda iko katika janga la kushuka daraja kwani hadi sasa inashikilia nafasi ya 15 ikiwa na pointi 23 na leo inamaliza michezo yake endapo ikifungwa itakuwa imeaga Ligi Kuu Bara 2017/18

Mrisho Ngasa atainusuru Ndanda leo!

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa