Samatta aongoza kwa ufungaji Ubelgiji

Na Mwandishi Wetu

Mshambuliajj wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga KRC Genk inayoshiriki Ligi kuu nchini Ubelgiji Mbwana Ali Samatta anaongoza kwa upachikaji magolj kwenye ligi ya nchi hiyo.

Samatta amefunga magoli manne wakati anayemfuatia amefunga magoli matatu, kung' ara kwa mshambuliajj huyo wa zamani wa African Lyon, Simba SC na TP Mazembe kunatokana na juhudi zake binafsi ambako kutamfanya apate soko haraka.

Samatta alijiunga na Genk mwanzoni mwa mwaka huu akitokea TP Mazembe ya DR Congo aliyoipa ubingwa wa Afrika, Samatta ndiye mwanasoka bora wa bara la Afrika kwa mwaka huu

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI