Kessy ruksa Yanga- TFF

Na Ikram Khamees, Dar es Salaam

Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) kupitia kamati yake ya Sheria na Hadhi za wachezaji leo imepitisha usajili wa vilabu vinavyoshiriki Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara (VPL) na Ligi Daraja la kwanza (FDL) huku ikipitisha jina la beki Hassan Ramadhan Kessy kuichezea Yanga msimu huu wa 2016/17.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Richard Sinamtwa amempitisha Kessy akidai alisajiliwa kihalali na hata madai ya klabu yake ya zamani ya Simba hayaendani na usajili wake, Kessy alisota benchi kwa muda mrefu baada ya klabu yake ya zamani ya Simba kumuwekea ngumu asicheze.

Hata hivyo mchezaji huyo akaanza kucheza kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii ambapo Yanga ilikutana na Azam FC Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, na katika mchezo huo Yanga ililala kwa mikwaju ya penalti 4-1 baada ya kumaliza dakika 90 kufungana mabao 2-2, Kessy alikosa penalti katika mchezo huo

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI