Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Staa Wetu: Mshamu Hassan "Mfuga Njiwa" Mtangazaji chipukizi wa mpira wa miguu, mwenye ndoto za kumfikia Juma Nkamia

Na Prince Hoza, Dar es Salaam

Anaitwa Mshamu Hassan lakini anajulikana zajdi kwa jina la Baba Nuraty Mfuga Njiwa, Ni mtangazaji wa redio Sibuka 94.5 FM inayosikika nchi nzima ikiwemo Dar es Salaam.

Mtangazaji huyo ameanza kujipatia umaarufu mkubwa kutokana na utangazaji wake kuvutia wengi na wale waliopata bahati ya kumsikia wamefurahishwa naye.

Alianza kazi hiyo akiwa kama mwanasalamu wa kawaida katika redio mbalimbali kiasi kwamba akajipatia umaarufu, Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu, Mfuga Njiwa alisema utangazaji ni kazi aliyoipenda ingawa hakupata kujua ataianzia wapi.

Salamu zilimwezesha kupata nafasi ya kujulikana na wengj na ndipo alipoweza kufanya interview katika vituo vya redio 13 na kimoja cha televisheni, Lakini anasema ni redio Sibuka pekee ndiyo iliyotambua kipaji chake.

Akaanza kazi katika redio hiyo na kipindi cha michezo cha kila siku cha Sportaiment na kile cha wiki kinachofanyika kila siku ya Jumamosi kiitwacho MBS ambavyo vyote anashiriki.

Pia Mfuga Njiwa amekuwa akipata nafasi ya kutangaza mpira wa miguu, Mtangazaji huyo ameanza kusikika katika mechi kadhaa za kirafiki na zile za Ligi kuu bara zinazofanyika katika viwanja mbalimbali hapa nchini.

Mfuga Njiwa aliyepata elimu yake ya msingi na sekondari Temeke Dar es Salaam  alizaliwa katika hospitali ya Temeke mwaka 1983, baba yake ni mzaliwa wa Mikindani mkoani Mtwara wakati mama yake ni mzaliwa wa Kilwa mkoani Lindi.

Mtangazaji huyo chipukizi ana ndoto kubwa za kumfikia mtangazaji mkongwe Juma Nkamia ambaye kwa sasa ni mbunge, Nkamia alikuwa akitangaza vema mpira wa miguu alipokuwa katika redio ya TBC Taifa.

Kwa wale waliobahatika kumsikia wanakiri kabjsa kuwa Mfuga Njiwa ni Nkamia wa pilj kwani ana kasi kubwa anapotangaza na akionekana kama mzoefu, aidha mtangazaji huyo huwa sambamba na wenzake David Pasko, John Ndeki, Salama Ngale, Omary Juma na mwingine anayefahamika kwa jina la Promise

Mfuga Njiwa akiwa kazini
Akiwa studio akifanya yake

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limetoa orodha ya viwango vya ubora wa klabu barani, Simba ikiendelea kuwa juu ya klabu nyingine za Tanzania, nafasi ya tano. Orodha hiyo imetoka leo kuelekea droo ya hatua za awali za michuano ya klabu Afrika ambayo kwa mara ya kwanza kihistoria itafanyika nchini katika studio za Azam Tv, Tabata Jijini Dar es Salaam. Yanga ambayo kama Simba itashiriki Ligi ya Mabingwa — yenyewe inashika nafasi ya 12, wakati timu nyingine katika orodha hiyo ni Namungo FC wanaoshika nafasi ya mwisho, ya 75 kwa pamoja na Salitas FC ya Burkina Faso, Ahli Benghazi ya Libya na NAPSA Stars ya Zambia. Kwa msimu ujao mbali na Simba na Yanga kushiriki Ligi ya Mabingwa, Azam FC na Singida Black Stars zitashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa