Yanga na GSM Foundation zatoa msaada kwa watoto Botswana
Uongozi wa Klabu ya kwa kushirikiana na GSM Foundation leo umetembelea kituo cha Ramotswa Centre for Deaf Education na kuwapatia mahitaji mbalimbali kwa ajili ya kituo hicho.
Kituo hiki kinatoa huduma za makazi (boarding) na malezi ya awali kwa watoto wenye changamoto za kusikia, kwa lengo la kuwasaidia kupata elimu, malezi na mazingira bora ya kukua na kujiendeleza.









