Simba yajipigia Mighty Wonderers 6-1
Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Ligi ya mabingwa Afrika Simba jioni ya leo imetinga raundi ya kwanza kwa kibabe baada ya kuifunga Mighty Wonderers mabao 6-1 na kuhitimisha kwa jumla ya mabao 7-1.
Ikishinda leo katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, Simba iliandikisha mabao yake kupitia viungo washambuliaji wake Clatous Chama aliyefunga mabao mawili, Libasse Gueye naye mawili, Morice Abraham na Keletso Makgalwa.
Bao pekee la Mighty Wonderers limefungwa kwa mkwaju wa penalti na Anold Emmanuel
