Seleman Mwalimu amjibu Chama
Baada ya Clatous Chama kudai kuwa Seleman Mwalimu huenda akawa anajutia kujiunga na Yanga SC baada ya kuikataa Simba, mshambuliaji huyo ameibuka na kutoa majibu.
Mwalimu amesema yupo na furaha kubwa Yanga na haoni sababu ya kulalamika, akisisitiza kuwa anafurahia maisha yake ndani ya klabu hiyo.
“Kaka nipo na furaha sanaaaaaaa na enjoy kuwa hapa Yanga ya moto mzee. Wanasema nilalamike kwa kipi mzee? Huku maisha safi, Hamdullilah na enjoy kuwa hapa.”
— Seleman Mwalimu kupitia Instagram
