Pacome awatakia kila kheri Yanga

Kiungo mshambuliaji aliyekwenye maumivu Pacome Zouzoua amewatumia salamu Watanzanis hasa klabu yake ya Yanga.

"Kila la kheri familia nzima ya Yanga kwenye safari ya Ligi ya Mabingwa. Isivyo bahati kutokuwepo kwangu kunanizuia mimi kuwa nanyi dimbani, lakini moyo wangu na fikra zipo pamoja nanyi”

Ni sehemu ya andiko la nyota wa Yanga SC, Pacome Zouzoua akiitakia heri timu yake ambayo leo itaanza mikikimikiki ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United ya nchini Botswana.

Pacome amewataka wachezaji wenzake kujitoa kwa kila hali ili kuipambania jezi yao na kuongeza kuwa atakuwa pamoja nao hata kama yeye yupo mbali.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI