Mimi sijawahi kufikiria suala la kwenda Yanga - Chama
Kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Zambia, Clatous Chama wa Simba ya Tanzania, amefunguka yafuatayo kwamba hakuwahi kuwaza wala kuota kucheza Yanga ila ilitokea tu.
"Nashukuru Mungu sikuchukua muda mrefu pale kwasababu sijawahi kufikiria suala la kwenda Yanga, ilitokea tu”
“Nilikuwa kwenye wakati mgumu lakini ninachoweza kusema ni kwamba, nimerudi Simba na siku niliyosaini Simba nilifurahi
sana hata familia yangu ilifurahi”
