Manqoba ashangazwa na waandishi
Kocha Mkuu wa Yanga SC, Manqoba Mngqithi, amesema ameshangazwa na idadi kubwa ya waandishi wa habari waliofika uwanjani kwa wakati mmoja.
Mngqithi amesema katika kipindi chote ambacho amekuwa akifanya kazi ya ukocha, hajawahi kuona waandishi wengi wa habari wakifika uwanjani kwa wakati mmoja kama ilivyokuwa leo.
“Tangu nianze kazi ya ukocha, sijawahi kuona waandishi wengi wa habari wakifika uwanjani kwa wakati mmoja kama nilivyoona leo.
Hata kwenye fainali za Klabu Bingwa Barani Afrika haijawahi kutokea waandishi wa habari wakifika uwanjani kutafuta habari kwa idadi kubwa kama leo.”
