Kocha wa Yanga ashinda tuzo ya mwezi

Kocha wa Young Africans, Manqoba Mngqithi, ametangazwa kuwa Kocha Bora wa mwezi Agosti katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/27, baada ya kuiongoza timu hiyo kufanya vizuri katika michezo ya mwezi huo.

Mngqithi aliiongoza Yanga kushinda michezo yote mitano iliyocheza mwezi Agosti, matokeo yaliyoiwezesha timu hiyo kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu.

Katika mchakato wa kuwania tuzo hiyo, Mngqithi aliwashinda Steve Barker wa Simba na Florent Ibenge wa Azam FC, ambao pia walikuwa wameingia hatua ya mwisho ya kinyang’anyiro hicho.


Machapisho maarufu kutoka blogu hii

FIFA yatoa orodha ya vilabu bora duniani, Simba na Yanga zachuana vikali

Kocha Simba anataka wachezaji wapya watano

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI