Depu hakamatiki
Mshambuliaji Aurelio Laurindo Depu ameendelea kung’ara katika Ligi ya Mabingwa Afrika (CAF Champions League), baada ya kufunga bao na kutoa assist katika sare ya 2-2 kati ya Petro de Luanda na UD de Songo jana.
Katika mchezo wa kwanza, Petro de Luanda ilishinda 1-0 dhidi ya UD de Songo, huku Depu akifunga bao pekee la mchezo. Kwa matokeo ya jumla ya 3-2, Depu amehusika moja kwa moja katika mabao yote matatu ya Petro de Luanda katika michezo hiyo miwili.
