Ajali ya bodaboda yaondoa uhai kipa wa Azam FC U20
MCHEZAJI wa Azam FC U-20, Iddy Salim, amefariki dunia baada ya kupata ajali ya pikipiki jana Alhamisi, Septemba 10, 2026.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Klabu ya Azam FC, marehemu alikuwa akicheza nafasi ya kipa katika timu ya vijana chini ya umri wa miaka 20 (U-20).
Mwili wa marehemu kwa sasa umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwananyamala (MRRH), ambapo unafanyiwa taratibu za mwisho kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Tanga kwa ajili ya maziko.
Azam FC pia imetuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu kufuatia msiba huo.
